Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 14:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kweli, kweli ninawaambia: yeye anayeniamini atafanya vilevile matendo ninayofanya. Na zaidi ya ile atafanya matendo makubwa kuliko haya, kwa sababu ninakwenda kwa Baba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 14:12
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: mukimwamini Mungu pasipo kuwa na shaka, hamutaweza kufanya tu kama nilivyotendea muti huu, lakini vilevile mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Ondoka hapa, ujitupe katika bahari,’ na itakuwa vile.


Akaona kwa mbali muti wa tini wenye majani mengi. Basi akaenda kuangalia kama atapata matunda juu ya muti ule. Lakini alipofika karibu nao, hakuona kitu juu yake isipokuwa majani matupu, kwa sababu haikukuwa wakati wake wa kutoa matunda.


Nao wote watakaoniamini watafanya vitambulisho hivi: watafukuza pepo kwa jina langu; watasema kwa luga mupya;


Mumesikia jinsi nilivyowaambia kwamba ninajiendea, lakini nitawarudilia tena. Kama mungenipenda, mungefurahia kujua kwamba ninakwenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mukubwa kuliko mimi.


Lakini mimi ninawaambia ukweli: ni faida kwenu mimi niende, kwa maana nisipokwenda, Musaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, nitamutuma kwenu.


Kwa maana neno hili ni kweli: ‘Mutu mumoja anapanda na mwingine anavuna.’


Kwa maana Baba anamupenda Mwana, anamwonyesha yote anayofanya yeye mwenyewe. Atamwonyesha mambo makubwa zaidi kuliko haya kusudi mupate kushangaa.


Yesu akasema: “Ningali pamoja nanyi kwa wakati kidogo na kisha nitarudi kwa yule aliyenituma.


(Alisema vile juu ya Roho atakayepokelewa na wale wanaomwamini Yesu. Kwa wakati ule Roho alikuwa hajatumwa bado, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.)


Kwa maana waliwasikia wakisema kwa luga za ajabu na kumutukuza Mungu. Halafu Petro akasema:


Naye akafanya hivi kwa muda wa siku nyingi. Na kwa mwisho Paulo akachukizwa naye. Basi akageuka na kumwambia yule pepo: “Ninakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, utoke ndani yake!” Na saa ile ile yule pepo akatoka ndani yake.


Na hata watu walitwaa vitambaa na nguo zilizogusa mwili wa Paulo, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakapona na pepo wakatoka ndani yao.


Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.


Siku ile watu waliosadiki mafundisho ya Petro, wakabatizwa. Na kadiri ya watu elfu tatu wakaongezeka katika kundi la wanafunzi.


wakisema: “Tutafanya nini na watu hawa? Wakaaji wote wa Yerusalema wanajua kwamba wameonyesha vitambulisho, nasi hatuwezi kukana jambo lile.


Nao mitume walishuhudia ufufuko wa Bwana Yesu kwa uwezo mukubwa, na Mungu akawabariki wote sana.


Lakini wengi kati ya watu waliosikia mafundisho ya Petro na Yoane wakaamini. Kadiri ya watu elfu tano wakaongezeka katika kundi la waamini.


Na kufuatana na mambo yote yaliyotokea, watu waliwapeleka wagonjwa katika barabara, wakiwalalisha juu ya mikeka na vipoyi kusudi Petro atakapopita, kivuli chake kipate tu kufika kwenye wamoja wao.


Basi Neno la Mungu likazidi kuenea katika Yerusalema na hesabu ya wanafunzi ikaongezeka sana kule na makuhani wengi wakaamini.


Maana pepo walitoka ndani ya watu wengi wakilalamika kwa sauti kubwa, na watu wengi wenye kupooza pamoja na viwete waliponyeshwa vilevile.


Petro akamwambia: “Ainea, Yesu Kristo anakuponyesha. Simama, ujitandikie kitanda chako wewe mwenyewe.” Na mara moja Ainea akasimama.


Petro akawaamuru watu wote waende inje, akapiga magoti na kuomba. Kisha akaelekea ile maiti na kusema: “Tabita, simama!” Halafu Tabita akafungua macho, na wakati alipomwona Petro akaamuka na kuikaa.


kwa njia ya uwezo wa vitambulisho na maajabu, na kwa uwezo wa Roho Mutakatifu. Hivi tokea Yerusalema mpaka kufika katika jimbo la Iliriko nimehubiri fasi zote Habari Njema ya Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ