Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 14:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Hauamini kwamba mimi na baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu na mimi ndani yake? Maneno ninayowaambia siyasemi kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini Baba anayekaa ndani yangu ndiye anayefanya kazi zake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 14:10
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini kama nikiyatenda, hata ikiwa hamuniamini mimi, basi mwamini matendo yangu, kusudi mupate kujua kabisa kwamba mimi na Baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu, nami ndani yake.”


Vilevile yeyote anayeishi ndani yangu na kuniamini, hatakufa hata milele. Unaamini maneno haya?”


Kwa maana sikusema kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini Baba aliyenituma ndiye aliyeniagiza maneno nitakayosema na kuyafundisha.


Muniamini wakati ninaposema kama mimi ni ndani ya Baba na Baba ni ndani yangu. Kama si vile, mwamini kwa sababu ya matendo niliyofanya.


Na wakati ule mutafahamu kwamba mimi ni ndani ya Baba yangu, na ninyi ni ndani yangu, na mimi ndani yenu.


Asiyenipenda hashiki maneno yangu. Na neno munalosikia nikisema halitoki kwangu, lakini linatoka kwa Baba yangu aliyenituma.


kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”


Lakini Yesu akawajibu: “Baba yangu anatumika wakati wote, nami ninatumika vilevile.”


Basi Yesu akaongeza kuwaambia Wayuda: “Kweli, kweli, ninawaambia: Mwana hawezi kufanya kitu kwa mafikiri yake mwenyewe; anafanya tu kile ambacho anaona Baba akifanya. Na mambo yote Baba anayofanya, Mwana anayafanya vilevile.


Yesu akawajibu: “Mafundisho ninayotoa si yangu, lakini ni ya yule aliyenituma.


Halafu Yesu akawaambia: “Wakati mutakapomunyanyua Mwana wa Mutu juu, mutafahamu kwamba ‘Mimi Ndimi.’ Na zaidi ya hii mutatambua kwamba sifanyi neno lolote kwa mapenzi yangu, lakini ninasema tu yale niliyofundishwa na Baba.


Mimi ninasema yale niliyoona kwa Baba yangu, lakini ninyi munafanya yale muliyosikia kutoka kwa baba yenu.”


Lakini sasa munatafuta kuniua ijapokuwa nimewaambia ukweli niliousikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya vile.


Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.


Ndiyo kusema, Mungu ndiye aliyekuwa akipatanisha watu wote na yeye mwenyewe kwa njia ya Kristo bila kuhesabu makosa yao. Yeye ametupatia ujumbe wa upatanisho.


Kwa maana Mungu mwenyewe alitaka ukamilifu wake uonekane ndani ya mwana wake.


Kwa maana ukamilifu wote wa Mungu uko ndani ya Kristo katika mwili wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ