Mufalme Yosafati akauliza: “Hakuna nabii yeyote hapa wa Yawe ambaye tunaweza kumwuliza shauri la Yawe?” Mutumishi mumoja wa mufalme Yoramu wa Israeli akajibu: “Elisha mwana wa Safati iko hapa. Yeye alikuwa mutumishi wa Elia.”
Heri watumishi wale bwana wao atakaowakuta wakikesha wakati anapofika! Kweli ninawaambia: atafunga mukaba wake vizuri na kuwakaribisha kula chakula, na kubakia pale akiwashugulikia.
“Tuseme kwa mufano, kati yenu kuna mutu mumoja anayekuwa na mutumishi anayemulimia au kumuchungia nyama wake. Mutumishi yule anaporudia toka kwenye shamba ataweza kumwambia kwamba aikae mara moja kula chakula?
Si vile, yeye atamwambia kwanza amupigie chakula na kujitayarisha vizuri kusudi amushugulikie mpaka atakapomaliza kula na kunywa. Kisha pale, ataweza kula na kunywa.
Kwa maana, ni nani anayekuwa mukubwa; yule anayeikaa kwa kula chakula au yule anayemushugulikia? Hakika ni yule anayeikaa kwa kula chakula. Ingawa vile mimi niko hapa katikati yenu kama mwenye kushugulika!
Kwa maana munajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ingawa alikuwa tajiri, yeye mwenyewe alijifanya masikini kwa ajili yenu, kusudi mupate kuwa watajiri kwa njia ya umasikini wake.