Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 13:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Ninawapa amri mupya: mupendane ninyi kwa ninyi. Kama mimi nilivyowapenda, nanyi mupendane vilevile.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 13:34
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mimi ni rafiki ya wote wanaokuheshimu, rafiki ya wanaoshika kanuni zako.


Na juu ya waaminifu katika inchi, ninaheshimu nguvu zao.


Usijilipize kisasi au kuwa na kinyongo juu ya wazao wa watu wako lakini umupende mwenzako kama vile unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ni Yawe.


Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.


Amri ninawapa ni kwamba mupendane ninyi kwa ninyi.


Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.


Mupendane ninyi kwa ninyi kwa kweli kama vile wandugu, nanyi muheshimiane ninyi kwa ninyi.


Anayemupenda mwenzake hawezi kumutendea vibaya. Basi Sheria inatimizwa kwa njia ya upendo.


Musikuwe na deni la mutu yeyote. Deni moja munalopaswa kuwa nalo ni kupendana. Kwa maana yule anayemupenda mwenzake ametimiza Sheria kabisa.


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,


Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.


Basi, tunapokuwa bado na wakati, tufanye mema kwa watu wote, na zaidi kwa wandugu zetu katika imani.


Musaidiane ninyi kubeba mizigo yenu, na hivi mutatimiza sheria ya Kristo.


Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.


Hayo yote ni kwa maana tumesikia namna munavyomwamini Yesu Kristo na namna munavyowapenda watu wote wa Mungu.


Na Bwana awaongezee na kuwazidishia upendo munaokuwa nao ninyi kwa ninyi na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tunavyowapenda ninyi.


Wandugu, tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu. Inatufaa kufanya vile kwa maana imani yenu inaongezeka, nao upendo wenu ninyi kwa ninyi unazidi kuongezeka.


Munafanya vizuri kama mukitimiza sheria hii ya kifalme inayopatikana katika Maandiko Matakatifu: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe.”


Ninyi mumekwisha kutakaswa kwa njia ya kutii neno la kweli kwa kuwapenda wandugu zenu pasipo unafiki. Basi mupendane kabisa, kwa moyo wenu wote.


undugu juu ya kushikamana na ibada, na upendo juu ya undugu wenu.


Kwa maana huu ndio ujumbe muliosikia tangia mbele: tupendane sisi kwa sisi.


Amri yake ndiyo hii tuamini jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane sisi kwa sisi kama vile Kristo alivyotuamuru.


Basi hii ndiyo amri tuliyopewa na Kristo: yule anayemupenda Mungu anapaswa kumupenda ndugu yake vilevile.


Na sasa Mama, ninakusihi: tupendane. Basi hii si amri mupya ninayokuandikia, lakini ni amri ile tuliyopokea tangu mwanzo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ