Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 13:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yesu alijua kwamba Baba yake ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, na kwamba yeye mwenyewe alitoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 13:3
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


“Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


Kulikuwa kumebaki siku moja mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kutoka katika dunia na kurudi kwa Baba yake imetimia. Yeye alikuwa akiwapenda watu wake waliokuwa katika dunia, na akaendelea kuwapenda mpaka mwisho.


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


Na zaidi ya hii hakuna mutu aliyepanda mbinguni, isipokuwa Mwana wa Mutu aliyeshuka toka mbinguni.


Baba anamupenda Mwana wake, naye ameweka vitu vyote kwa mukono wake.


lakini mimi ninamujua sababu nilitoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”


Yesu akasema: “Ningali pamoja nanyi kwa wakati kidogo na kisha nitarudi kwa yule aliyenituma.


Yesu akawajibu: “Hata nikijishuhudia mimi mwenyewe, ushuhuda wangu ni wa kweli, kwa sababu ninajua pahali nilipotoka na pahali ninapokwenda. Lakini ninyi hamujui pahali nilipotoka wala pahali ninapokwenda.


Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mungenipenda, kwa maana nimetoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini yeye ndiye aliyenituma.


“Kwa hiyo watu wa taifa la Israeli wajue hakika kwamba yule Yesu muliyemutundika juu ya musalaba, Mungu amemufanya kuwa Bwana na Masiya!”


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu aliweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Ndiyo Maandiko Matakatifu yanasema kwamba alipewa mamlaka juu ya vitu vyote. Lakini maneno haya yanaonyesha wazi kwamba Mungu hahesabiwi katika hili neno “Vyote”, kwa maana ni yeye aliyemupa mamlaka juu ya vitu vyote.


Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ