Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 13:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Na kulikuwa mumoja wa wanafunzi ambaye Yesu alimupenda, na aliyekuwa akimwegamia Yesu pale kwenye chakula.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 13:23
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini yule masikini alikuwa na mwana-kondoo mudogo mumoja dike, ambaye alikuwa amemununua. Alimutunza, naye akakomaa katika nyumba yake pamoja na watoto wake. Alimukulisha mwana-kondoo yule chakula kilekile kama chake na kunywea kwenye kikombe chake naye vilevile alikuwa akimukumbatia kwenye kifua. Mwana-kondoo yule alikuwa kama binti kwa yule mutu masikini.


Siku moja yule masikini akakufa, na wamalaika wakamupeleka mpaka pembeni ya Abrahamu. Na yule tajiri akakufa vilevile na kuzikwa.


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


Hawa wadada wawili wakatuma habari hii kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako mupendwa ni mugonjwa.”


Halafu Wayuda wamoja wakasema: “Angalia namna alivyomupenda kweli!”


Yesu aliwapenda Marta na dada yake pamoja na Lazaro.


Basi Simoni Petro akamukonyezea yule mwanafunzi jicho kusudi amwulize Yesu ni nani anayemusema.


Halafu yule mwanafunzi akamwegamia Yesu na kumwuliza: “Bwana, ni nani?”


Basi wakati Yesu alipoona mama yake pale na yule mwanafunzi aliyemupenda, akisimama karibu, akamwambia mama yake: “Mama, sasa huyu ndiye mwana wako.”


Basi akaenda mbio kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine aliyependwa na Yesu na kuwaambia: “Wameondoa maiti ya Bwana toka katika kaburi na hatujui pahali walipoiweka.”


Petro akageuka, akaona nyuma yao mwanafunzi yule aliyependwa na Yesu. (Ni yeye aliyeegamia kifua cha Yesu wakati wa chakula na kumwuliza: “Bwana, ni nani yule atakayekutoa?”)


Ni huyu huyu mwanafunzi ndiye aliyeshuhudia mambo hayo na kuyaandika; nasi tunajua kwamba ushuhuda wake ni wa kweli.


Halafu mwanafunzi yule aliyependwa na Yesu akamwambia Petro: “Ni Bwana.” Simoni Petro aliposikia kwamba ni Bwana, akavaa kanzu yake (kwa maana alikuwa havai kitu), naye akajitupa ndani ya maji.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ