Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 13:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Ninawaambia ninyi sasa hayo yote mbele hayajatokea, kusudi wakati yatakapotokea, mwamini kwamba ‘Mimi Ndimi.’

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 13:19
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutuambie yatakayotokea nyuma, nasi tujue basi kama ninyi ni miungu. Mufanye kitu chochote, chema au kibaya, kusudi tushangae na kuogopa.


Ninyi Waisraeli ni washuhuda wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwachagua mukuwe watumishi wangu, mupate kunijua na kuniamini, kwamba mimi ni Mungu. Mbele yangu hakukuwa mungu mwingine, wala hakutakuwa mungu mwingine nyuma yangu.


Kwa hiyo nilikutangazia mambo yale tangu zamani, mbele hayajatukia, mimi nilikujulisha, kusudi usiseme: Ni sanamu yangu iliyotenda mambo hayo, sanamu zangu za chuma ndizo ziliyaagiza.


Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.


kumwuliza Yesu: “Wewe ndiwe yule aliyepaswa kuja kutuokoa au tumungojee mwingine?”


Yoane alimushuhudia akisema kwa sauti: “Huyu ndiye niliyesema juu yake: ‘Anayekuja nyuma yangu ananipita, kwa sababu alikuwa mbele sijazaliwa.’ ”


Nimewaambia maneno haya sasa mbele hayajatokea, kusudi wakati yatakapotokea, mupate kuamini.


Lakini ninawaambia maneno haya kusudi wakati ule utakapotimia mupate kukumbuka kwamba nimekwisha kuwaambia. “Sikuwaambia ninyi maneno hayo mbele kwa sababu nilikuwa ningali pamoja nanyi.


Yesu akamujibu: “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”


Halafu Yesu akawaambia: “Wakati mutakapomunyanyua Mwana wa Mutu juu, mutafahamu kwamba ‘Mimi Ndimi.’ Na zaidi ya hii mutatambua kwamba sifanyi neno lolote kwa mapenzi yangu, lakini ninasema tu yale niliyofundishwa na Baba.


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: mbele Abrahamu hajazaliwa, mimi nilikuwa niko.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ