Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 13:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 “Sisemi juu ya ninyi wote; ninawajua wale niliowachagua. Lakini inafaa maneno haya yanayosemwa na Maandiko Matakatifu yatimie: ‘Yule aliyechangia chakula nami, amenigeuka.’

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 13:18
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua; hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”


Isimaeli mwana wa Netania pamoja na wale watu kumi, wakasimama na kumushambulia kwa upanga Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, wakamwua. Gedalia ndiye aliyekuwa amesimikwa na mufalme wa Babeli kuwa mutawala wa inchi.


na adui wa mutu atakuwa wa jamaa yake mwenyewe.


Nao walipokuwa wakikula, akasema: “Kweli ninawaambia: mumoja kati yenu atanitoa.”


Yesu akajibu: “Yule aliyechovya mukate pamoja nami ndani ya sahani ndiye atanitoa.


Ilipokuwa magaribi, Yesu akafika pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.


Walipokuwa wameikaa kula chakula, Yesu akasema: “Kweli ninawaambia: mumoja kati yenu anayekula pamoja nami atanitoa.”


Yesu akawajibu: “Ni mumoja kati yenu ninyi kumi na wawili, anayechovya mukate pamoja nami ndani ya sahani moja.


“Lakini muangalie: yule anayenitoa anachangia chakula pamoja nami.


Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akafazaika na kusema: “Kweli, kweli ninawaambia, mumoja wenu atanitoa.”


Wanafunzi wakaangaliana, kwa maana hawakujua ni nani Yesu aliyemusema.


Yesu akajibu: “Nitachovya kipande cha mukate. Yule nitakayemupa kipande kile ndiye yeye.” Basi Yesu akachovya kipande cha mukate na kumupa Yuda mwana wa Simoni Iskariota.


Ninyi hamukunichagua mimi, lakini ni mimi niliyewachagua ninyi. Nami nimewatuma muende kuzaa matunda yasiyokuwa na mwisho. Kwa hiyo Baba atawapa chochote munachoomba kwa jina langu.


Kama mungekuwa watu wa dunia, dunia ingewapenda, kwa maana ninyi ni watu wake. Lakini nimewachagua ninyi toka dunia hii, na ninyi si watu wa dunia tena. Ni kwa sababu hii dunia inawachukia.


Lakini wamefanya hivi kusudi maneno haya yaliyoandikwa katika Sheria yao yatimie: ‘Wamenichukia pasipo sababu.’


Wakati nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda kwa uwezo wa jina lako, ndilo lile jina ulilonipa. Nimewachunga wala hakuna mumoja wao aliyepotea, isipokuwa yule anayepaswa kupotea, kusudi Maandiko Matakatifu yatimizwe.


(Ilifanyika hivi kusudi litimie lile neno Yesu alilosema kwa kuonyesha kifo gani atakachokufa.)


Waaskari wakaambiana: “Tusipasue kanzu hii, lakini tuipigie kura, kusudi tujue itakuwa ya nani.” Mambo haya yalifanyika kusudi Maandiko Matakatifu yanayosema hivi yatimie: “Waligawanya nguo zangu nayo kanzu yangu wakaipigia kura.” Mambo hayo ndiyo waaskari waliyofanya.


Mambo haya yalifanyika kusudi Maandiko Matakatifu yanayosema hivi yatimie: “Hakuna hata mufupa wake mumoja utakaovunjwa.”


Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.


Yesu akawajibu: “Ni mimi peke niliyewachagua ninyi kumi na wawili, lakini ingawa hivi mumoja wenu ni Shetani!”


“Wandugu zangu, ilikuwa lazima yale Maandiko Matakatifu yatimie ambayo Roho Mutakatifu alitabiri kwa kinywa cha mufalme Daudi juu ya Yuda, yule aliyewaongoza wale waliomukamata Yesu.


mpaka siku ile aliponyanyuliwa mbinguni. Mbele ya kunyanyuliwa kule, alitoa maagizo kwa njia ya Roho Mutakatifu kwa watu aliokuwa amewachagua kuwa mitume wake.


Kwa maana, hatutangazi habari zetu sisi wenyewe, lakini tunatangaza kwamba Yesu Kristo ndiye Bwana, nasi tuko watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.


Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ