Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 13:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Sasa kwa kuona munajua jambo hili, mutakuwa wenye heri kama mukilifanya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 13:17
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Noa akafanya yote kama vile Mungu alivyomwamuru.


Yanatamanika kuliko zahabu, kuliko zahabu safi kabisa. Ni matamu kuliko asali, kuliko asali safi kabisa.


Basi, Musa alitimiza kwa ukamilifu kabisa maagizo yote ya Yawe.


Pasipo maono ya kinabii, watu wanashindwa kujizuiza. Heri mutu yule anayeshika sheria.


Yawe akaniambia: Tangaza maneno hayo yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema. Uwaambie watu wayasikilize masharti ya agano hili na kuyashika.


Nitatia roho yangu ndani yenu; nitawafanya mufuate masharti yangu na kushika maagizo yangu.


Kwa maana yeyote anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa katika mbingu, huyu ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”


Lakini Yesu akajibu: “Heri zaidi wale wanaosikia neno la Mungu na kulitii!”


Ninyi ni warafiki zangu, kama mukifanya sawa ninavyowaagiza.


Ni vile kwa sababu si wale wanaosikia Sheria ndio wanaohesabiwa haki mbele ya Mungu, lakini ni wale wanaotii Sheria.


Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.


Lakini mutu anayechunguza sheria kamilifu inayoweka watu huru na kuendelea kushikamana nayo, na si kuisikia tu na kisha kuisahau, lakini anaitimiza kabisa, mutu huyu atabarikiwa na Mungu katika shuguli zake.


Basi, mutu anayejua kutenda mema wala hayatendi, anafanya zambi.


Heri wale wanaosafisha kanzu zao, kwa maana watakuwa na haki ya kukula matunda ya muti wa uzima na ya kuingia katika muji ule kwa kupitia kwenye milango.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ