Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 12:49 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

49 Kwa maana sikusema kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini Baba aliyenituma ndiye aliyeniagiza maneno nitakayosema na kuyafundisha.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 12:49
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hauamini kwamba mimi na baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu na mimi ndani yake? Maneno ninayowaambia siyasemi kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini Baba anayekaa ndani yangu ndiye anayefanya kazi zake.


Asiyenipenda hashiki maneno yangu. Na neno munalosikia nikisema halitoki kwangu, lakini linatoka kwa Baba yangu aliyenituma.


lakini sherti dunia ijue kama ninamupenda Baba, nami ninafanya kama alivyoniagiza. “Musimame, tutoke hapa.


Siwaiti ninyi tena watumishi, kwa sababu mutumishi hajui mambo bwana wake anayofanya. Ninawaita ninyi warafiki kwa sababu nimewajulisha yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu.


kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Kweli, kweli ninakuambia: tunasema maneno tunayojua na kushuhudia maneno tuliyoona, lakini ninyi hamutaki kupokea ushuhuda wetu.


anashuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna mutu anayekubali ushuhuda wake.


Basi Yesu akaongeza kuwaambia Wayuda: “Kweli, kweli, ninawaambia: Mwana hawezi kufanya kitu kwa mafikiri yake mwenyewe; anafanya tu kile ambacho anaona Baba akifanya. Na mambo yote Baba anayofanya, Mwana anayafanya vilevile.


“Siwezi kufanya kitu kwa mafikiri yangu mwenyewe. Ninahukumu tu kama vile Mungu anavyoniambia na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu sitafuti kufanya mapenzi yangu, lakini mapenzi ya yule aliyenituma.


Simoni Petro akamujibu: “Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unasema maneno ya uzima wa milele.


Yesu akawajibu: “Mafundisho ninayotoa si yangu, lakini ni ya yule aliyenituma.


Nina maneno mengi ya kusema juu yenu na ya kuwahukumu. Lakini yule aliyenituma ni wa kweli, nami ninajulisha dunia maneno yale niliyosikia kwake.”


Halafu Yesu akawaambia: “Wakati mutakapomunyanyua Mwana wa Mutu juu, mutafahamu kwamba ‘Mimi Ndimi.’ Na zaidi ya hii mutatambua kwamba sifanyi neno lolote kwa mapenzi yangu, lakini ninasema tu yale niliyofundishwa na Baba.


Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mungenipenda, kwa maana nimetoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini yeye ndiye aliyenituma.


Nitawachagulia kati ya wandugu zao wenyewe nabii kama wewe, nitatia maneno yangu ndani ya kinywa chake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.


Hizi ni habari za mambo yaliyofunuliwa na Yesu Kristo. Kristo alipata ufunuo huu kutoka kwa Mungu, kusudi awaonyeshe watumishi wake mambo yanayopaswa kutokea kisha kidogo. Kristo alimutuma malaika wake kwa kumujulisha mutumishi wake Yoane mambo yale.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ