Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa mufalme wa Misri. Mimi nimefanya moyo wake kuwa mugumu na wa wakubwa wake kusudi nipate kuonyesha vitambulisho hivi kati yao,
Basi, Musa na Haruni walifanya maajabu hayo yote mbele ya mufalme wa Misri. Lakini Yawe alifanya moyo wa mufalme kuwa mugumu, akakataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke katika inchi yake.
Mimi nitafanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu, nao watawafuatilia katikati ya bahari. Nami nitajipatia utukufu kutokana na kuangamizwa kwa mufalme wa Misri na jeshi lake, magari yake ya vita pamoja na wapanda-farasi wake.
Halafu mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye atawafuatilia. Nami nitajipatia utukufu kwa kumwangamiza yeye na jeshi lake. Halafu Wamisri watatambua kwamba mimi ni Yawe.” Basi, Waisraeli wakafanya hivyo.
Yawe akamwambia Musa: “Utakapofika Misri, uhakikishe kwamba umetenda mbele ya mufalme wa Misri miujiza yote niliyokupa uwezo wa kuifanya. Lakini mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye hatawaachilia Waisraeli waondoke.
Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!
Lakini aliumizwa kwa sababu ya zambi zetu, alipondwa kwa sababu ya maovu yetu. Kwa kuazibiwa kwake sisi tumepata uzima; kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
Kisha akaniambia: Ufanye akili za watu hawa kuwa ngumu, masikio yao yasisikie, macho yao yasione; wasipate kuona kwa macho yao, wasipate kusikia kwa masikio yao, wasipate kuelewa kwa akili zao, na kunigeukia, nao wapate kupona.
Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu, mimi nitawaponyesha ukosefu wenu wa uaminifu. Nanyi munasema: Sisi tunarudi kwako, maana wewe ndiwe Yawe, Mungu wetu.
Na ikiwa nabii yule akidanganyika na kusema kitu, basi mimi Yawe nimemupotosha. Nami nitanyoosha mukono wangu kwa kumwondoa nabii yule kutoka kwa watu wangu Waisraeli.
Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.
Halafu watasema: Tuende tumurudilie Yawe! Yeye mwenyewe ameturarua, lakini yeye mwenyewe atatuponyosha. Yeye mwenyewe ametuumiza, lakini yeye mwenyewe atatunza vidonda.
“Roho wa Bwana yuko pamoja nami, maana amenichagua niwahubirie wamasikini Habari Njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kwamba watakombolewa nao vipofu kwamba wataona. Amenituma kuwapa wanaoteswa uhuru,
Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa Mungu, lakini kwa watu wengine si vile. Wao wanaambiwa maneno hayo kwa njia ya mifano, kusudi waangalie, lakini wasione kitu, nao wasikie, lakini wasifahamu kitu.”
Kanisa liliwapatia vitu walivyohitaji kwa ajili ya safari ile, nao wakapita katika inchi ya Foinikia na katika Samaria. Na kule wakaeleza namna watu wa mataifa mengine walivyomugeukia Mungu. Habari hii ikafurahisha sana wandugu waamini wote.
Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.