Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 12:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Na lile kundi la watu wakamujibu: “Sisi tumesikia katika maandiko ya Sheria kwamba Kristo ataishi milele. Basi namna gani unaweza kusema kama Mwana wa Mutu anapaswa kunyanyuliwa juu? Na huyu Mwana wa Mutu ni nani?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 12:34
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu na kiti chake cha kifalme cha ufalme wake nitakiimarisha milele.


Yawe amekuapia hivi wala hatabadilisha nia yake: “Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”


Haki istawi maisha yake yote, na amani kwa wingi mpaka mwezi ukome.


Alikamatwa kwa kinguvu, akahukumiwa na kupelekwa kuuawa; na hakuna mutu aliyejali mambo yanayomupata. Alifukuzwa kutoka inchi ya wanaokuwa wazima, kwa sababu ya makosa ya watu wangu.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme, kusudi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote wamutumikie. Utawala wake ni wa milele na ufalme wake hautaangamizwa hata kidogo.


Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.


Hao waliolemewa ndio watakaobaki wazima; hao waliopelekwa katika uhamisho watakuwa taifa lenye nguvu. Yawe atawatawala kwenye mulima Sayuni, tangu wakati ule na hata milele.


Yesu alipofika pande za muji Kaisaria Filipi, akawauliza wanafunzi wake: “Watu wanasema kwamba Mwana wa Mutu ni nani?”


Yesu alipoingia Yerusalema, muji wote ukavuma. Watu wakaulizana: “Huyu ni nani?”


Yesu akamujibu: “Mbweha wako na makao yao ndani ya matundu, nao ndege wako na chicha, lakini Mwana wa Mutu hana nafasi ya kulala.”


Yesu akawajibu: “Imeandikwa katika sheria yenu kwamba Mungu amesema: ‘Ninyi ni miungu.’


Lakini mimi, nitakaponyanyuliwa toka katika dunia, nitawavuta watu wote kuja kwangu.”


Lakini wamefanya hivi kusudi maneno haya yaliyoandikwa katika Sheria yao yatimie: ‘Wamenichukia pasipo sababu.’


Halafu Yesu akawaambia: “Wakati mutakapomunyanyua Mwana wa Mutu juu, mutafahamu kwamba ‘Mimi Ndimi.’ Na zaidi ya hii mutatambua kwamba sifanyi neno lolote kwa mapenzi yangu, lakini ninasema tu yale niliyofundishwa na Baba.


Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.


Basi kama vile kosa la mutu mumoja limewaletea watu wote azabu, ni hivi vilevile tendo la haki la mutu mumoja limewaweka huru na kuwapa uzima.


Lakini Yesu hawezi kukombolewa kwa kazi yake ya ukuhani, kwa sababu yeye anaishi kwa milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ