Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 12:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Kulikuwa Wagriki wamoja kati ya wale watu waliofika Yerusalema kuabudu wakati wa sikukuu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 12:20
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Mwanamuke yule hakukuwa wa taifa la Wayuda. Alikuwa muzaliwa wa jimbo la Foinikia, katika inchi ya Suria. Yeye akamwomba Yesu afukuze yule pepo kutoka ndani ya binti yake.


Siku sita mbele ya Pasaka, Yesu alifika Betania, kwao Lazaro, yule mutu Yesu aliyemufufua.


Basi Wafarisayo wakasemezana hivi: “Hamwoni kwamba hatuwezi kufanya kitu? Angalia, dunia nzima inamufuata!”


Wayuda wakaulizana hivi wao kwa wao: “Mutu huyu atakwenda wapi sisi tusipoweza kumwona? Ataenda kwa Wayuda waliosambazwa kati ya Wagriki na kuwafundisha Wagriki?


Paulo na Barnaba walipofika katika muji Ikonio, wakaingia vilevile katika nyumba ya kuabudia ya Wayuda. Mule wakahubiri hata kundi kubwa la Wayuda na mataifa mengine wakaamini.


Paulo akafika Derbe na Listra, ambako kulikuwa mwanafunzi mumoja aliyeitwa Timoteo. Mama yake alikuwa Muyuda, naye alikuwa ameamini lakini baba yake alikuwa Mugriki.


Wamoja kati ya Wayuda wakasadiki na kujiunga pamoja na Paulo na Sila. Vilevile kundi kubwa la Wagriki walioogopa Mungu pamoja na wanawake wengi wenye heshima wakasadiki.


Nimewaonya Wayuda wa mataifa mengine kwamba wanapaswa kumugeukia Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.


wakilalamika: “Ninyi wanainchi Waisraeli, mutusaidie! Huyu ndiye mutu yule anayefundisha kwa watu wote, nafasi zote maneno ya kuzarau taifa letu, Sheria ya Musa, na hekalu hili. Na zaidi ya hii, amewaingiza watu wa mataifa mengine katika hekalu na hivi amechafua Pahali hapa Patakatifu!”


Basi Filipo akajitayarisha na kwenda. Alipokuwa katika njia, mara moja akakutana na towashi mumoja Mwetiopia. Mutu huyu alikuwa mukubwa, alishugulika na kazi ya usimamizi wa mali zote za malkia Kandake wa Etiopia. Yeye alikuwa amekwenda Yerusalema kwa kumwabudu Mungu,


Mimi sisikii haya juu ya Habari Njema, kwa sababu huo ndio uwezo wa Mungu unaowaokoa wote wanaoamini, kwanza Wayuda na kisha watu wa mataifa mengine vilevile.


Basi hakuna tofauti kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kwa maana Bwana wa wote ni mumoja tu, na anawabariki sana wote wanaomusihi.


Na Tito aliyesafiri pamoja nami hakulazimishwa kutahiriwa ingawa alikuwa Mugriki,


Kwa hiyo hakuna tena umbalimbali kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kati ya watumwa na watu huru, mwanaume na mwanamuke; kwa maana ninyi wote ni mumoja katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Kwa hiyo hakuna tena tofauti kati ya watu wa mataifa mengine na Wayuda, wenye kutahiriwa na wasiotahiriwa, wageni, washenzi, watumwa na watu huru. Lakini Kristo ni yote naye yuko katika wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ