Vuma, ewe upepo wa kaskazini, kuja, ewe upepo wa kusini, muvume juu ya bustani yangu, mujaze anga kwa marasi, mupenzi wangu akuje katika bustani yake akule matunda yake bora kuliko yote.
Yesu alikuwa Betania katika nyumba ya mutu aliyeitwa Simoni Mukoma. Walipokuwa wakikula, mwanamuke mumoja akaingia ndani ya nyumba. Alikuwa na chupa la jiwe lenye marasi ya bei kali yaliyotengenezwa na maua ya nardo safi. Kisha akavunja mudomo wa lile chupa na kumimia marasi juu ya kichwa cha Yesu.
Heri watumishi wale bwana wao atakaowakuta wakikesha wakati anapofika! Kweli ninawaambia: atafunga mukaba wake vizuri na kuwakaribisha kula chakula, na kubakia pale akiwashugulikia.
Kwa maana, ni nani anayekuwa mukubwa; yule anayeikaa kwa kula chakula au yule anayemushugulikia? Hakika ni yule anayeikaa kwa kula chakula. Ingawa vile mimi niko hapa katikati yenu kama mwenye kushugulika!
Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami.