Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 12:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Wanafunzi wake hawakuelewa maneno haya kwanza, lakini wakati Yesu alipokwisha kutukuzwa, wakakumbuka kwamba maneno haya yameandikwa juu yake na ni vile walivyomutendea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 12:16
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Bwana Yesu alipokwisha kusema nao maneno hayo, akanyanyuliwa juu kwenda mbinguni na kuikaa kwa upande wa kuume wa Mungu.


Lakini wanafunzi hawakufahamu maana ya mafundisho hayo. Wakaogopa kumwuliza neno.


Wanafunzi wake hawakufahamu maana ya maneno hayo, kwa sababu yalikuwa yamefichwa kwao, nao hawakutambua kama Yesu alisema juu ya nini.


Basi Yesu akawaambia: “Enyi wajinga na wenye mioyo mizito kwa kuamini maneno yote manabii waliyosema!


Halafu akawafungua akili kusudi wapate kufahamu Maandiko Matakatifu


Lakini wao hawakufahamu maana ya maneno hayo, kwa sababu yalikuwa yamefichwa kwao, kusudi wasipate kuyatambua. Nao waliogopa kumwuliza maana yake.


Yesu akawajibu: “Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mutu imetimia.


Lakini Musaidizi, ndiye Roho Mutakatifu, yule Baba atakayemutuma kwa jina langu, atawafundisha maneno yote na kuwakumbusha yote niliyowaambia.


Lakini ninawaambia maneno haya kusudi wakati ule utakapotimia mupate kukumbuka kwamba nimekwisha kuwaambia. “Sikuwaambia ninyi maneno hayo mbele kwa sababu nilikuwa ningali pamoja nanyi.


Na sasa, Baba, unipe utukufu karibu nawe, utukufu unaokuwa sawa na ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuumbwa kwa dunia.


Wakati Yesu alipokwisha kufufuka, wanafunzi wake wakakumbuka kwamba alikuwa anasema juu ya jambo lile, wakaamini Maandiko Matakatifu na maneno yale aliyosema.


(Alisema vile juu ya Roho atakayepokelewa na wale wanaomwamini Yesu. Kwa wakati ule Roho alikuwa hajatumwa bado, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.)


Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.


“Kwa hiyo watu wa taifa la Israeli wajue hakika kwamba yule Yesu muliyemutundika juu ya musalaba, Mungu amemufanya kuwa Bwana na Masiya!”


Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Jambo la lazima sana katika maneno tunayosema sasa ni hili. Tuko na Mukubwa wa namna ile, anayeikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mwenyezi Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ