Mufalme akamwuliza Siba: “Kwa nini umeleta vitu hivi?” Siba akamujibu: “Punda ni kwa ajili ya kubeba watu wa jamaa yako, mikate na matunda ni kwa ajili ya vijana wote, nayo divai ni kwa ajili ya wale watakaochoka katika jangwa.”
Nawe kilima cha Yerusalema, wewe munara wa Sayuni, ambamo Mungu anafanya ulinzi juu ya watu wake, kama muchungaji juu ya kondoo wake, wewe utakuwa tena muji wenye mamlaka sawa zamani. Yerusalema utakuwa tena muji mukubwa wa mufalme.
Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.
“Muwaambie wakaaji wa muji Sayuni: ‘Angalia, mufalme wenu anakuja kwenu. Yeye ni munyenyekevu, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, kitoto cha punda.’ ”
Hata hivyo, asikuwe na farasi wengi kwa ajili yake mwenyewe, wala asiwarudishe watu Misri kwa kujipatia farasi zaidi, kwa sababu Yawe amewaonya: ‘Hamutarudi tena kwa njia ile.’
Yeye alikuwa na watoto wanaume makumi ine na wajukuu makumi tatu ambao walipanda juu ya punda makumi saba. Alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka minane.