57 Nao wakubwa wa makuhani na Wafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mutu akijua pahali Yesu alipokuwa, alete habari kusudi wapate kumufunga.
Ingawa niliwapenda, walinishitaki. Hata hivyo, niliwaombea.
Wakajaribu tena kumufunga Yesu, lakini akawaponyoka.
Lakini wengine kati yao wakawaendea Wafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyofanya.
Basi wakubwa wa makuhani na Wafarisayo wakakusanya Baraza yao Kubwa, na kusema: “Tufanye nini kwa kuona mutu huyu anaonyesha vitambulisho vingi?
Kwa ajili ya hii, wakaokota mawe kwa kumutupia. Lakini Yesu akajificha na kutoka ndani ya hekalu.
Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliogopa wakubwa wa Wayuda. Wakubwa wale walikuwa wamekwisha kupatana kwamba mutu yeyote anayesadiki kuwa Yesu ndiye Kristo, atatengwa asiingie katika nyumba ya kuabudia.