Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 11:55 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

55 Sikukuu ya Wayuda ya Pasaka ilikuwa karibu. Basi watu wengi toka katika vijiji wakaenda Yerusalema kusudi wajitakase mbele ya Pasaka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 11:55
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yakobo akawaambia jamaa yake na wote aliokuwa nao: “Mutupilie mbali sanamu za miungu ya kigeni munazokuwa nazo, mujitakase na kubadilisha nguo zenu.


Kila mara karamu ilipomalizika, Yobu aliita wana wake kusudi awatakase. Aliamuka asubui mapema kisha karamu, akatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya kila mumoja wao maana aliwaza: “Labda wana wangu wametenda zambi na kumutukana Mungu ndani ya mioyo yao.”


Ninanawa mikono yangu kuonyesha kama sina kosa, na kuizunguka mazabahu yako, ee Yawe,


Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa watu uwatakase leo na kesho. Uwaambie wafue nguo zao


Mumoja wenu au mumoja wa wazao wenu akiwa muchafu kwa sababu amegusa maiti au akiwa mbali katika safari, lakini akiwa anataka kunifanyizia sikukuu ya Pasaka,


Lakini, watu wamoja waliokuwa pale walikuwa hawawezi kushiriki sikukuu hiyo ya Pasaka kwa sababu walikuwa wamegusa maiti, wakakuwa wachafu. Hao waliwaendea Musa na Haruni,


Yesu alipomaliza kusema maneno hayo yote, akawaambia wanafunzi wake:


“Munajua kwamba kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mutu apate kutolewa kusudi atundikwe juu ya musalaba.”


Kulikuwa kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka na ya Mukate Usiyotiwa Chachu. Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walitafuta njia ya kumukamata Yesu kwa werevu kusudi wamwue.


Sikukuu ya Mukate Usiotiwa Chachu, inayoitwa Pasaka, ilikaribia.


Siku sita mbele ya Pasaka, Yesu alifika Betania, kwao Lazaro, yule mutu Yesu aliyemufufua.


Kulikuwa kumebaki siku moja mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kutoka katika dunia na kurudi kwa Baba yake imetimia. Yeye alikuwa akiwapenda watu wake waliokuwa katika dunia, na akaendelea kuwapenda mpaka mwisho.


Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.


Wakati sikukuu ya Pasaka ya Wayuda ilipokaribia, Yesu akaenda Yerusalema.


Pale kulikuwa mitungi sita iliyotengenezwa kwa mawe iliyotumiwa na Wayuda kwa kutilia maji ya kujitakasa. Ndani ya kila mumoja kuliweza kuingia yapata litre mia moja za maji.


Nyuma ya maneno hayo, Yesu akaenda Yerusalema kwa sikukuu ya Wayuda.


Na Pasaka, ambayo ni moja ya sikukuu za Wayuda, ilikuwa karibu.


Kwenda ujiunge na watu wale katika ibada ya utakaso, nawe uwalipie malipo yanayoamuriwa kusudi wapate kunyolewa. Hivi watu wote watajua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako zilikuwa za uongo mutupu. Na zaidi ya hii watajua kwamba unafuata Sheria ya Musa katika maisha yako.


Halafu kesho yake Paulo akaenda na wale watu wane, na akajitakasa pamoja nao. Kisha akaingia ndani ya hekalu na kutangaza wakati siku za utakaso zitakapotimia, na sadaka itakayotolewa kama malipo kwa ajili ya kila mumoja wao.


Na wakati ule nilipokuwa nikifanya mambo hayo, walinikuta katika hekalu, nami nilikuwa nimekwisha kufanya ibada ya kutakaswa. Sikukuwa na kundi la watu wala kuleta fujo.


Basi kila mutu ajichunguze mwenyewe na kisha akule mukate huu na kunywa kikombe hiki.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


Samweli akawajibu: “Nimekuja kwa amani. Nimekuja kumutolea Yawe sadaka. Mujitakase wenyewe halafu tuende kutolea sadaka.” Samweli akamutakasa Yese pamoja na wana wake, akawakaribisha kwenye sadaka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ