Basi, Yakobo akawaambia jamaa yake na wote aliokuwa nao: “Mutupilie mbali sanamu za miungu ya kigeni munazokuwa nazo, mujitakase na kubadilisha nguo zenu.
Kila mara karamu ilipomalizika, Yobu aliita wana wake kusudi awatakase. Aliamuka asubui mapema kisha karamu, akatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya kila mumoja wao maana aliwaza: “Labda wana wangu wametenda zambi na kumutukana Mungu ndani ya mioyo yao.”
Mumoja wenu au mumoja wa wazao wenu akiwa muchafu kwa sababu amegusa maiti au akiwa mbali katika safari, lakini akiwa anataka kunifanyizia sikukuu ya Pasaka,
Lakini, watu wamoja waliokuwa pale walikuwa hawawezi kushiriki sikukuu hiyo ya Pasaka kwa sababu walikuwa wamegusa maiti, wakakuwa wachafu. Hao waliwaendea Musa na Haruni,
Kulikuwa kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka na ya Mukate Usiyotiwa Chachu. Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walitafuta njia ya kumukamata Yesu kwa werevu kusudi wamwue.
Kulikuwa kumebaki siku moja mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kutoka katika dunia na kurudi kwa Baba yake imetimia. Yeye alikuwa akiwapenda watu wake waliokuwa katika dunia, na akaendelea kuwapenda mpaka mwisho.
Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.
Pale kulikuwa mitungi sita iliyotengenezwa kwa mawe iliyotumiwa na Wayuda kwa kutilia maji ya kujitakasa. Ndani ya kila mumoja kuliweza kuingia yapata litre mia moja za maji.
Kwenda ujiunge na watu wale katika ibada ya utakaso, nawe uwalipie malipo yanayoamuriwa kusudi wapate kunyolewa. Hivi watu wote watajua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako zilikuwa za uongo mutupu. Na zaidi ya hii watajua kwamba unafuata Sheria ya Musa katika maisha yako.
Halafu kesho yake Paulo akaenda na wale watu wane, na akajitakasa pamoja nao. Kisha akaingia ndani ya hekalu na kutangaza wakati siku za utakaso zitakapotimia, na sadaka itakayotolewa kama malipo kwa ajili ya kila mumoja wao.
Na wakati ule nilipokuwa nikifanya mambo hayo, walinikuta katika hekalu, nami nilikuwa nimekwisha kufanya ibada ya kutakaswa. Sikukuwa na kundi la watu wala kuleta fujo.
Samweli akawajibu: “Nimekuja kwa amani. Nimekuja kumutolea Yawe sadaka. Mujitakase wenyewe halafu tuende kutolea sadaka.” Samweli akamutakasa Yese pamoja na wana wake, akawakaribisha kwenye sadaka.