Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 11:42 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

42 Na ninajua kwamba unanisikia siku zote, lakini ninasema hivi kwa sababu ya watu hawa wanaokusanyika hapa kusudi wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 11:42
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Haujui kwamba ninaweza kumwomba Baba yangu musaada na mara moja angenitumia zaidi ya makundi kumi na mawili ya wamalaika?


Lakini ninajua kwamba hata sasa, kitu chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”


Wakati wale Wayuda waliokuwa ndani ya nyumba pamoja na Maria kwa kumufariji walipomwona akisimama upesi na kutoka, wakamufuata. Walizani kama anakwenda kulia kwenye kaburi.


Wakati alipokwisha kusema maneno haya, akaita kwa sauti kubwa, akisema: “Lazaro, toka inje.”


kwa maana kwa ajili yake Wayuda wengi walijitenga nao na kumwamini Yesu.


Wale watu wote waliokuwa pamoja na Yesu wakati alipomwita Lazaro toka ndani ya kaburi na kumufufua walishuhudia mambo yaliyofanyika.


Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.


Baba mwenye haki, ijapokuwa dunia haikujui, mimi ninakujua na hawa wanajua kwamba ulinituma.


kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Lakini hii imeandikwa kusudi mupate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mupate uzima katika jina lake.


Mungu hakumutuma Mwana wake katika ulimwengu kusudi ahukumu ulimwengu, lakini kusudi ulimwengu uokolewe naye.


Lakini hata ningehukumu, hukumu yangu ingekuwa ya kweli, kwa sababu sihukumu peke yangu, lakini Baba aliyenituma ni pamoja nami.


Yule aliyenituma ni pamoja nami; hakuniacha peke yangu, kwa sababu siku zote ninafanya maneno yanayomupendeza.”


Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mungenipenda, kwa maana nimetoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini yeye ndiye aliyenituma.


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemutuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ