Yesu akawakazia macho kwa kasirani, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wao. Akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, nao ukakuwa muzima tena.
Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu! Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”
Wakati wale Wayuda waliokuwa ndani ya nyumba pamoja na Maria kwa kumufariji walipomwona akisimama upesi na kutoka, wakamufuata. Walizani kama anakwenda kulia kwenye kaburi.
“Sasa roho yangu inafazaika. Nami sijui niseme nini. Nimwombe Baba, aniokoe toka mambo yale yatakayofika saa hii? Hapana, kwa sababu nimefika kwa ajili ya yale yatakayofanyika saa hii.
Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.