Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 11:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Wayuda wengi walikuwa wamekuja kwa Marta na Maria kwa kuwafariji kwa ajili ya kifo cha kaka yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 11:19
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watoto wake wanaume na wanawake wakamufikia kwa kumufariji, lakini akakataa kufarijiwa, akisema: “Uniache. Nitaendelea kuomboleza kwa ajili ya mwana wangu, mpaka nitakaposhuka katika kaburi.” Ndivyo baba yake alivyomulilia.


Mufalme Daudi akasema: “Nitamutendea mema Hanuni mwana wa Nahasi kama vile baba yake alivyonitendea mimi.” Halafu, Daudi akatuma wajumbe kumupa pole kwa ajili ya kifo cha baba yake. Nao wajumbe wa Daudi walipofika katika inchi ya Waamori,


mashujaa wote wakaondoka na kutwaa mwili wa Saulo na miili ya wana wake, wakaileta mpaka Yabesi. Wakazika mifupa yao chini ya muti wa mwalo kule Yabesi, nao wakafunga kula kwa muda wa siku saba.


Warafiki watatu wa Yobu walisikia juu ya hasara zote zilizomupata Yobu, wakaamua kwa pamoja waende kumupa pole na kumufariji. Majina yao ni: Elifasi kutoka inchi ya Temani, Bildadi wa inchi ya Suhi na Zofari wa inchi ya Namati.


Kisha wandugu zake, wadada zake na warafiki wote waliomufahamu mbele wakamwendea kwake, wakakula chakula pamoja naye. Wakamupa pole na kumufariji kwa ajili ya mateso yote ambayo Yawe alikuwa amemuletea. Kila mumoja wao akamupa Yobu feza na pete ya zahabu.


Afazali kwenda kwenye kilio, kuliko kwenda kwenye karamu, kwa sababu inawapasa wenye kuwa wazima kukumbuka kwamba kifo kinawangojea sisi wote.


Hasara hizi mbili zimekupata: uharibifu na maangamizi; njaa na mauaji. Nani atakayekuonea huruma? Nani atakayekufariji?


Kwa sababu ya hayo ninalia, machozi yananitiririka, sina mutu yeyote wa kunifariji; hakuna yeyote wa kunitia moyo. Watoto wangu wameachwa ukiwa, maana adui yangu amenishinda.


Unalia usiku kucha; machozi yanatiririka juu ya mashavu yake. Hakuna hata mumoja kati ya wapenzi wake kwa kuufariji. Rafiki zake wote wameudanganya; wamekuwa waadui zake.


Sikiliza ninavyolalamika; hakuna wa kunifariji. Waadui zangu wote wamesikia juu ya taabu yangu: wanafurahi kwamba umeniletea hasara. Uifanye ile siku uliyoahidi ifike, uwafanye nao wateseke kama mimi.


Uchafu wake ulionekana waziwazi, lakini muji wenyewe haukujali mwisho wake. Anguko lake lilikuwa kubwa sana; hakuna anayeweza kuufariji. Unasema: Angalia, ee Yawe, mateso yangu, maana adui yangu ameshinda.


Nikuambie nini, ee Yerusalema? Nikulinganishe na nini? Nikufananishe na kitu gani kusudi niweze kukufariji, ee Sayuni uliyekuwa muzuri? Maangamizi yako ni mengi kama bahari, ni nani atakayekuponyesha?


Marta alikuwa na dada yake mudogo aliyeitwa Maria. Huyo aliikaa mbele ya Bwana, akisikiliza mafundisho yake.


Kuna kitu kimoja tu cha lazima. Maria amechagua kitu kinachokuwa kizuri zaidi ambacho hakuna mutu atakayekiondoa kwake.”


Huu ndio ushuhuda wa Yoane kwa makuhani na Walawi waliotumwa na Wayuda kutoka Yerusalema kumwuliza kwamba yeye ni nani.


Kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Lazaro, muzaliwa wa Betania aliyepatwa na ugonjwa. Wadada zake Maria na Marta walikaa katika kijiji kile.


Wakati wale Wayuda waliokuwa ndani ya nyumba pamoja na Maria kwa kumufariji walipomwona akisimama upesi na kutoka, wakamufuata. Walizani kama anakwenda kulia kwenye kaburi.


Wakati Yesu alipomwona akilia, na wale Wayuda waliokuja pamoja naye wakilia vilevile, akasisimua kwa huzuni nyingi na kufazaika.


Halafu Wayuda wamoja wakasema: “Angalia namna alivyomupenda kweli!”


Wayuda wengi kati ya wale waliokuja kwa Maria, na walioona mambo Yesu aliyofanya, wakamwamini.


Wanafunzi wakamwambia: “Mwalimu, hakujapita siku nyingi tokea pale Wayuda walipotaka kukutupia mawe, na sasa unataka kwenda tena kule!”


Mufurahi pamoja na wenye kufurahi. Mulie pamoja na wenye kulia.


Yeye anatufariji katika taabu yetu yote, kusudi tupate kuwafariji wale wanaokuwa katika taabu yoyote kwa kuwaletea faraja tuliyopokea kutoka kwa Mungu.


Basi mufarijiane na kujengana imani, kama vile munavyozoea kufanya.


Kisha, wakaitwaa mifupa yao na kuizika chini ya muti wa mukwaju kule Yabesi, nao wakafunga kula chakula kwa muda wa siku saba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ