Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 10:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yesu aliwaambia mufano huu, lakini hawakuelewa maneno aliyosema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 10:6
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Babu zetu walipokuwa Misri, hawakujali matendo ya ajabu ya Mungu; hawakukumbuka wingi wa wema wake, lakini walimwasi kando ya bahari Nyekundu.


“Lakini ninyi hamujui wala hamufahamu! Ninyi munatembea katika giza la upotovu! Misingi yote ya haki katika dunia imetikiswa!


Waovu hawaelewi haki ya sheria, lakini wanaomwogopa Yawe wanaielewa kabisa.


Hao ni kama imbwa walafi sana, wala hawawezi kutosheka hata kidogo. Wachungaji nao hawana akili yoyote. Kila mumoja anatafuta njia yake mwenyewe, kila mumoja anatafuta faida yake.


Watu wengi wataondolewa uchafu, watatakaswa na kusafishwa. Lakini watu waovu wataendelea kutenda uovu. Hakuna hata mumoja wa hao waovu atakayeelewa; wenye hekima ndio watakaoelewa.


Yesu aliwaambia makundi ya watu maneno hayo yote akitumia mifano. Yeye hakusema nao pasipo kutumia mifano.


Yesu akawauliza watu: “Mumeelewa maneno hayo yote?” Nao wakamujibu: “Ndiyo.”


Hakusema nao pasipo kutumia mifano lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao, aliwafasiria mambo yote.


“Nimewaambia ninyi maneno hayo kwa mifano. Lakini kutakuwa wakati sitasema nanyi tena kwa mifano, lakini nitawaambia ninyi waziwazi juu ya Baba.


Basi wanafunzi wake wakamwambia: “Sasa unasema waziwazi pasipo kutumia mifano.


Basi Wayuda wakaanza kubishana sana kati yao, wakasema: “Namna gani mutu huyu anaweza kutupatia mwili wake tuukule?”


Wengi kati ya wanafunzi wake waliposikia maneno haya, wakasema: “Masemi haya ni magumu. Ni nani anayeweza kuyakubali?”


Yeye anasema kwamba tutamutafuta, lakini hatutamwona, na kwamba hatuwezi kufika pahali atakapokwenda. Maana ya maneno haya ni gani?”


Kwa sababu gani hamuelewi maneno ninayowaambia? Ni kwa sababu hamutaki kusikia maneno yangu.


Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


Kile kitu walichofanya kinaonyesha wazi mufano unaosema: “Imbwa amerudilia kula matapiko yake,” na: “Nguruwe aliyesafishwa amerudia tena kugaagaa katika matope!”


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ