42 Na kule watu wengi wakamwamini Yesu.
Wayuda wengi kati ya wale waliokuja kwa Maria, na walioona mambo Yesu aliyofanya, wakamwamini.
Hata hivi wengi kati ya wakubwa wa Wayuda wakamwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Wafarisayo, hawakushuhudia kwamba wameamini. Waliogopa kwamba watatengwa wasiingie katika nyumba ya kuabudia.
Wakati ule Yesu alipokuwa Yerusalema kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini kwa sababu waliona vitambulisho alivyofanya.
Wasamaria wengi wa muji ule walimwamini Yesu kwa sababu ya maneno ya yule mwanamuke aliposhuhudia hivi: “Aliniambia mambo yote niliyotenda.”
Wengine wengi zaidi waliamini kwa sababu ya maneno yake mwenyewe,
Watu wengi katika kundi lililokuwa pale wakamwamini, wakisema: “Kristo atakapokuja, ataonyesha vitambulisho zaidi kuliko mutu huyu?”
Alipokuwa akisema maneno haya, watu wengi wakamwamini.