Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 10:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

33 Wayuda wakamujibu: “Hatutaki kukutupia mawe kwa ajili ya tendo zuri, lakini kwa sababu unamutukana Mungu. Wewe ni mutu tu, lakini unajifanya kuwa Mungu!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 10:33
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, mutafute watenda maovu wawili wapate kumushuhudia na kumushitaki wakisema: ‘Wewe umemutukana Mungu na mufalme.’ Kisha mumupeleke inje, mumwue kwa kumutupia mawe!”


Mimi nilisema kwamba ninyi ni miungu, kwamba ninyi wote ni wana wa Mungu Mukubwa!


Umuondoe kijana aliyetukana inje ya kambi, wale wote waliomusikia akitukana waweke mikono yao juu ya kichwa chake, na wote pamoja wamwue kwa kumupiga mawe.


Mutu yeyote akuwe ni mwenyeji au mugeni anayemutukana Yawe, wote pamoja watamwua kwa kumupiga mawe.


Halafu Wayuda wakamuzunguka, na kumwambia: “Mpaka wakati gani utatuzungusha kichwa? Kama wewe ni Kristo, utuambie waziwazi.”


Yesu akawaambia tena: “Nimewaonyesha matendo mengi mazuri kwa uwezo wa Baba. Ni kwa sababu ya tendo gani kati ya hayo munataka kunitupia mawe?”


Wayuda wakamujibu: “Kufuatana na moja ya sheria zetu, mutu huyu anapaswa kuuawa, kwa sababu alijiita Mwana wa Mungu.”


Kwa ajili ya neno hili Wayuda walitaka tena zaidi kumwua; si kwa sababu ya kuvunja Sheria ya siku ya Sabato tu, lakini vilevile kwa sababu alisema kwamba Mungu ni Baba yake, akijifanya hivi kuwa sawasawa na Mungu.


Kila mutu anapaswa kutii wakubwa wenye mamlaka. Maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; nao wakubwa wanaotawala wamesimikwa na Mungu.


Tangu mwanzo yeye alikuwa na hali ya Mungu, lakini hakuona kwamba kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ