Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 10:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Mimi na Baba yangu tuko mumoja.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 10:30
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Basi muwaendee watu wa mataifa yote kusudi wapate kuwa wanafunzi wangu, mukiwabatiza kwa jina la Baba, la Mwana na la Roho Mutakatifu.


Baba yangu aliyenipa kondoo hawa ni mukubwa kuliko wote, na hakuna mutu anayeweza kuwanyanganya toka kwa Baba yangu.


Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?


Yesu akamujibu: “Anayenipenda, atashika maneno yangu. Baba yangu atamupenda, naye Baba pamoja nami tutaingia ndani yake na kukaa ndani yake.


Yesu akajibu: “Filipo, nimekwisha kuwa nanyi siku nyingi sasa, nawe haujanijua bado? Aliyeniona mimi amemwona Baba. Basi sababu gani unasema: ‘Utuonyeshe Baba?’


Yote Baba anayokuwa nayo ni yangu. Ni kwa sababu hii nilisema kwamba maneno Roho atakayowaambia yatatokana na yale yanayokuwa ndani yangu.


Na yote ninayokuwa nayo ni yako, na yote unayokuwa nayo ni yangu, nami nimetukuzwa kwa njia yao.


Lakini Yesu akawajibu: “Baba yangu anatumika wakati wote, nami ninatumika vilevile.”


kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: mbele Abrahamu hajazaliwa, mimi nilikuwa niko.”


“Basi musikilize, enyi Waisraeli! Yawe, Yawe tu, ni Mungu wetu.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Na hivi tutaishi tukingojea ule uheri tunaoutumainia, wakati utukufu wa Mungu wetu Mukubwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo utakapotokea.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ