26 Lakini ninyi hamusadiki kwa sababu ninyi si kondoo wangu.
Kondoo wangu wanasikia sauti yangu, ninawajua, nao wananifuata.
Anapokwisha kuwatia hao kondoo wake inje, anawatangulia, nao wanamufuata kwa sababu wanajua sauti yake.
Wote Baba anaonipa wanakuja kwangu; nami sitamukataa hata kidogo yule anayekuja kwangu.
Yesu akaongeza kusema: “Kwa sababu hii niliwaambia kama hakuna mutu anayeweza kuja kwangu, isipokuwa anawezeshwa na Baba.”
Anayekuwa mutu wa Mungu anasikia maneno ya Mungu. Hamusikii, kwa sababu ninyi si watu wa Mungu.”
Lakini sisi ni watu wa Mungu. Mutu anayemujua Mungu anatusikiliza; yule asiyemujua Mungu hatusikilizi. Basi ni kwa njia hii tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho ya udanganyifu.