Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 10:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Yesu akawajibu: “Nimekwisha kuwaambia ninyi, lakini hamusadiki. Matendo ninayofanya kwa mamlaka ya Baba yananishuhudia mimi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 10:25
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yesu akawaambia tena: “Nimewaonyesha matendo mengi mazuri kwa uwezo wa Baba. Ni kwa sababu ya tendo gani kati ya hayo munataka kunitupia mawe?”


Kama sifanyi matendo ambayo Baba yangu ananiamuru, musiniamini.


Lakini kama nikiyatenda, hata ikiwa hamuniamini mimi, basi mwamini matendo yangu, kusudi mupate kujua kabisa kwamba mimi na Baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu, nami ndani yake.”


Basi wakubwa wa makuhani na Wafarisayo wakakusanya Baraza yao Kubwa, na kusema: “Tufanye nini kwa kuona mutu huyu anaonyesha vitambulisho vingi?


Ingawa vitambulisho vyote alivyoonyesha mbele yao, hawakumwamini,


Muniamini wakati ninaposema kama mimi ni ndani ya Baba na Baba ni ndani yangu. Kama si vile, mwamini kwa sababu ya matendo niliyofanya.


Yesu alionyesha vitambulisho vingine vingi mbele ya wanafunzi wake visivyoandikwa katika kitabu hiki.


Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”


Watu wengi katika kundi lililokuwa pale wakamwamini, wakisema: “Kristo atakapokuja, ataonyesha vitambulisho zaidi kuliko mutu huyu?”


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Ni kwa sababu hii niliwaambia ninyi kama mutakufa katika zambi zenu. Musipoamini kwamba ‘Mimi Ndimi’, hakika mutakufa katika zambi zenu.”


Baba yenu Abrahamu alishangilia akitumainia kuona siku ya kuja kwangu; na wakati alipoiona, alifurahi.”


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: mbele Abrahamu hajazaliwa, mimi nilikuwa niko.”


Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.


“Ninyi wanainchi wenzangu Waisraeli, musikilize maneno haya: Yesu wa Nazareti alikuwa mutu aliyetambulishwa wazi na Mungu mbele yenu kwa njia ya vitambulisho, miujiza, na maajabu aliyofanya katikati yenu kama munavyojua ninyi wenyewe.


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ