Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 10:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yesu akasema: “Kweli, kweli ninawaambia: mutu asiyeingia kwa mulango wa upango wa kondoo, lakini anapandia na kuingilia nafasi ingine, yeye ni mwizi na munyanganyi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 10:1
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, Yawe anasema hivi juu ya hao manabii: Wanatabiri kwa jina langu, ingawa mimi sikuwatuma. Wanasema kwamba hakutakuwa vita wala njaa katika inchi hii: Manabii hao wataangamia kwa vita na kwa njaa.


Yawe anaendelea kusema: Mimi sikuwatuma hao manabii, lakini wao walikwenda mbio; sikuwaambia kitu chochote, lakini wao walitabiri!


Vilevile mimi Yawe ninasema kwamba nitawashambulia manabii wanaotabiri ndoto zao za uongo kwa watu wangu, na kuwapotosha kwa uongo wao na upuuzi wao. Mimi sikuwatuma wala kuwaamuru waende, kwa hiyo hawatawafalia watu hao kitu. –Ni ujumbe wa Yawe!


Wanashambulia muji, wanakimbia juu ya ukuta; wanapanda juu ya nyumba na kuingia, wanapenya katika madirisha kama wezi.


“Mufanye angalisho na manabii wa uongo; kwa maana wanakuja kwenu wakionekana kwa inje kama vile kondoo, lakini ndani, wao ni kama imbwa wakali wa pori.


Basi Yesu akaongeza kusema: “Kweli, kweli ninawaambia: mimi ni mulango wa upango wa kondoo.


Yesu akamujibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”


Na namna gani watahubiri ikiwa hawatumwi? Ni kama inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Angalia jinsi kunavyofurahisha kuja kwa wale wanaoleta habari njema.”


Kwa maana watu wa namna hii hawamutumikii Bwana wetu Kristo, lakini wanatumikia tu tumbo yao wenyewe. Tena kwa maneno yao matamu na ya kujipendekeza wanadanganya watu wasiokuwa na makosa.


Inafaa kuwanyamazisha watu hao kwa sababu wanapotosha jamaa nzima kwa kufundisha mambo yasiyofaa wakitafuta kupata mali kwa njia mbaya.


Hakuna mutu anayejipatia heshima hii ya kuwa Kuhani Mukubwa yeye mwenyewe. Lakini anapaswa kuitwa na Mungu, kama vile Haruni alivyoitwa.


Manabii walifanya uchunguzi na upelelezi juu ya wokovu ule, nao walitabiri juu ya zawadi ambayo ninyi mungepewa.


Zamani manabii wa uongo walitokea kati ya watu, na ndivyo hivyo walimu wa uongo watakavyotokea kati yenu. Watu hawa wataingiza mafundisho mabaya sana ya uongo kwa siri, wakimukataa hata Bwana aliyewakomboa na kujiletea maangamizi upesi.


Na kwa sababu ya tamaa yao mbaya ya mali, walimu hawa wa uongo watajipatia faida juu yenu kwa njia ya maneno ya uongo. Lakini tangia zamani hukumu yao imekwisha kutangazwa, nao hawatakawia kuangamizwa.


Wapendwa wangu, musimwaminie kila mutu anayesema kwamba yuko na Roho wa Mungu, lakini mumupime kwa kuhakikisha kama roho yule anatoka kwa Mungu. Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea katika dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ