Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Ule mwangaza wa kweli, unaomwangazia kila mutu, unakuja katika dunia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 1:9
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.


Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.


Lakini kama macho yako yanaharibika, mwili wako wote utabaki katika giza. Basi ikiwa mwangaza unaokuwa ndani yako umegeuka kuwa giza, giza hilo ni nzito sana!


Basi kama mwili wako wote uko katika mwangaza pasipo kiungo kinachokuwa katika giza, mwili wako wote utabaki katika mwangaza kabisa, kama vile taa inavyokuangazia kwa mwangaza wake.”


Yeye alikuwa chemichemi ya uzima, na uzima huu ulikuwa mwangaza kwa watu.


Alikuja kushuhudia ule mwangaza kusudi watu wote wapate kuamini kwa njia yake.


Mimi nimekuja katika dunia kama mwangaza, kusudi mutu yeyote anayeniamini asikae katika giza.


Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


“Mimi ni muzabibu wa kweli, na Baba yangu ni mulimaji.


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: Musa hakuwapa ninyi mukate wa mbinguni, lakini ni Baba yangu anayewapa ninyi mukate wa kweli wa mbinguni.


Katika kundi lile kulikuwa manunguniko mengi juu yake. Wamoja walisema: “Yeye ni mutu muzuri.” Wengine walisema: “Hapana, si vile, yeye anawadanganya watu.”


Tukisema kwamba hatuna zambi, tunajidanganya sisi wenyewe, wala ukweli hauko ndani yetu.


Kwa ngambo ingine amri hii ninayowaandikia ni mupya, na ukweli wake unaonekana ndani ya Kristo na ndani yenu vilevile. Kwa maana giza linapita na mwangaza wa kweli umekwisha kutokea.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ