Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 1:45 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

45 Kisha Filipo akamukuta Natanaeli, akamwambia: “Tumemwona yule ambaye Musa aliandika habari zake katika kitabu cha Sheria na ambaye manabii walisema juu yake. Ni Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 1:45
41 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kutokana na wazao wako mataifa yote katika dunia yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu.”


Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Siku ile, tawi Yawe atakalochipuza litakuwa zuri na tukufu, nayo matunda ya inchi yatakuwa na heshima na utukufu kwa wale Waisraeli watakaobaki. Waisraeli watakaobaki watasifiwa na kujivunia mazao ya inchi yao.


Maana, mbele ya Yawe, mutumishi wake alikomaa kama kichipukizi, kama muzizi katika inchi kavu. Hakukuwa na umbo wala sura ya kupendeza, wala hakukuwa na uzuri wowote wa kutuvuta.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


na kumwambia kwamba Yawe wa majeshi anasema hivi: Hapa kuna mutu anayeitwa Tawi. Yeye atastawi pale anapokuwa na kulijenga hekalu la Yawe.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


kisha Filipo na Bartolomayo, Toma na Matayo aliyekuwa mulipishaji wa kodi; Yakobo mwana wa Alfayo, na Tadeo;


Huyu si mwana wa yule seremala? Mama yake si Maria? Nao Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda si wandugu zake?


Kule akakaa katika muji ulioitwa Nazareti, kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa mutu wa Nazareti.”


Kundi la watu wakajibu: “Huyu ni nabii Yesu wa Nazareti katika Galilaya.”


Alipomwona Petro akiota moto, akamwangalia, na kumwambia: “Wewe vilevile ulikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”


Huyu si yule museremala, mwana wa Maria, ndugu ya Yakobo, Yose, Yuda na Simoni? Nao wadada zake, si wanaishi hapa kati yetu?” Na kwa hiyo wakakosa kumwaminia.


Wakamwambia kwamba ni Yesu wa Nazareti ndiye anayepita.


Basi Yosefu naye vilevile akaondoka katika muji Nazareti, wa jimbo la Galilaya, na kwenda Yudea katika muji wa kuzaliwa wa mufalme Daudi, unaoitwa Betelehemu. Alienda kule kwa sababu alikuwa mutu wa ukoo wa Daudi.


Wazazi wake walipomwona, wakashangaa sana. Mama yake akamwuliza: “Mutoto wangu, kwa nini umetufanyia kama hivi? Mimi na baba yako tulikutafuta tukiwa na wasiwasi.”


Kisha akawaelezea maneno yaliyoandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu yote, akianza toka vitabu vya Musa na kuendelea katika vitabu vya manabii wote.


Kisha akawaambia: “Haya ndiyo maneno niliyowaambia wakati nilipokuwa ningali pamoja nanyi, kwamba sherti yatimizwe maneno yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Musa, katika maandiko ya manabii na katika Zaburi.”


Wakati Yesu alipoanza kazi yake alikuwa na umri wa miaka yapata makumi tatu. Yeye alizaniwa kuwa mwana wa Yosefu. Yosefu alikuwa mwana wa Heli, Heli alikuwa mwana wa Matati, Matati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yana, Yana alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Matatia, Matatia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esili, Esili alikuwa mwana wa Nage, Nage alikuwa mwana wa Mati, Mati alikuwa mwana wa Matatia, Matatia alikuwa mwana wa Simei, Simei alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yoda, Yoda alikuwa mwana wa Yoana, Yoana alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubali alikuwa mwana wa Saltieli, Saltieli alikuwa mwana wa Neri, Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri, Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Matati, Matati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea, Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matata, Matata alikuwa mwana wa Natani, Natani alikuwa mwana wa Daudi, Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nasoni, Nasoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesironi, Hesironi alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaka, Isaka alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori, Nahori alikuwa mwana wa Serugu, Serugu alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sela, Sela alikuwa mwana wa Kainana, Kainana alikuwa mwana wa Aripakisadi, Aripakisadi alikuwa mwana wa Semu, Semu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki, Lameki alikuwa mwana wa Metusela, Metusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahaleli, Mahaleli alikuwa mwana wa Kainana, Kainana alikuwa mwana wa Enosi, Enosi alikuwa mwana wa Seti, Seti alikuwa mwana wa Adamu, Adamu aliumbwa na Mungu.


Nao wote wakamufurahia na kushangaa na maneno mazuri aliyosema. Wakasema: “Huyu si mwana wa Yosefu?”


(Filipo alikuwa muzaliwa wa Betesaida, muji wa Andrea na Petro.)


Basi wakamwendea Filipo wa kijiji cha Betesaida ya Galilaya na kumwambia: “Bwana, tunataka kuonana na Yesu.”


Filipo akamwambia: “Bwana, utuonyeshe Baba, na ile itatutoshelea.”


Wakamujibu: “Yesu wa Nazareti.” Yesu akawaambia: “Ni mimi.” Na Yuda, yule aliyekuwa amemutoa, alikuwa akisimama pale pamoja nao.


Yesu akawauliza tena: “Munamutafuta nani?” Nao wakasema: “Yesu wa Nazareti.”


Pilato akaamuru andiko liandikwe na kuwekwa juu ya musalaba. Nalo liliandikwa hivi: “Yesu wa Nazareti, Mufalme wa Wayuda.”


Simoni Petro, Toma (anayeitwa Pacha), Natanaeli (wa muji Kana katika Galilaya), nao wana wa Zebedayo pamoja na wanafunzi wengine wawili wa Yesu, wote walikuwa pamoja.


Nao wakasema: “Huyu si Yesu mwana wa Yosefu? Si tunawajua baba yake na mama yake? Namna gani anaweza kusema sasa kwamba alishuka toka mbinguni?”


Wakati Yesu alipoinua macho, akaona kundi kubwa la watu wakimufikia. Halafu akamwuliza Filipo: “Wapi tunaweza kununua vyakula kwa kulisha watu hawa?”


Filipo akamujibu: “Hata tukinunua mikate kwa bei ya vikoroti mia mbili vya feza, haitatosha kwa kumupa kila mutu hata kidogo tu.”


Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.


“Ninyi wanainchi wenzangu Waisraeli, musikilize maneno haya: Yesu wa Nazareti alikuwa mutu aliyetambulishwa wazi na Mungu mbele yenu kwa njia ya vitambulisho, miujiza, na maajabu aliyofanya katikati yenu kama munavyojua ninyi wenyewe.


Nami nikauliza: ‘Wewe ni nani, Bwana?’ Na Bwana akanijibu: ‘Mimi ni Yesu wa Nazareti unayemutesa.’


“Kweli mimi mwenyewe niliwaza kwamba nilipaswa kufanya yote ninayoweza kwa kupinga jina la Yesu wa Nazareti.


Lakini Petro akamwambia: “Sina mali yoyote, lakini nitakupa kile ninachokuwa nacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ninakuamuru simama utembee!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ