Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 1:42 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

42 Kisha akamupeleka Simoni kwa Yesu. Yesu akamwangalia, akasema: “Wewe ndiwe Simoni mwana wa Yoane, sasa utaitwa Kefa.” (Jina “Kefa” ni sawasawa na “Petro” na maana yake ni “Jiwe.”)

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 1:42
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Namani alipopata habari hii, akaenda kwa mufalme na kumwelezea habari za mutoto yule.


Na haya ndiyo majina ya hao mitume wake kumi na wawili: kwanza Simoni (anayeitwa vilevile Petro) na ndugu yake Andrea; Yakobo na ndugu yake Yoane, ambao ni wana wa Zebedayo;


Wale kumi na wawili aliowachagua ni hawa: Simoni (Yesu aliyemupa jina la Petro),


Simoni Petro alipoona mambo hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu na kusema: “Bwana, utoke karibu nami, kwa sababu mimi ni mutu mwenye zambi!”


Simoni (Yesu aliyemupa jina la Petro) na ndugu yake Andrea, Yakobo na Yoane, Filipo na Bartolomayo,


“Sisemi juu ya ninyi wote; ninawajua wale niliowachagua. Lakini inafaa maneno haya yanayosemwa na Maandiko Matakatifu yatimie: ‘Yule aliyechangia chakula nami, amenigeuka.’


Simoni Petro, Toma (anayeitwa Pacha), Natanaeli (wa muji Kana katika Galilaya), nao wana wa Zebedayo pamoja na wanafunzi wengine wawili wa Yesu, wote walikuwa pamoja.


Yesu akamwambia: “Uende kumwita mume wako na urudi naye hapa.”


Ninataka kusema: kila mumoja kati yenu anasema maneno yake mbalimbali. Mumoja anasema: “Mimi ni wa Paulo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Petro,” na mwingine anasema: “Mimi ni wa Kristo.”


Alimutokea Petro, na kisha akawatokea mitume wake kumi na wawili.


ikiwa Paulo, Apolo au Petro, dunia, uzima, kifo, mambo ya sasa au mambo yatakayokuja.


Au sina haki ya kusafiri pamoja na mwanamuke mukristo kama vile mitume wengine wanavyofanya, nao wandugu za Bwana na hata Petro?


Kulipokwisha kupita miaka mitatu, nikaenda Yerusalema kusudi nipate kujuana na Petro, nami nikakaa kwake kwa muda wa siku kumi na tano.


Petro alipofika Antiokia, nilibishana naye waziwazi, kwa sababu alikuwa akidanganyika.


Basi Yakobo, Petro na Yoane, waliohesabiwa kuwa waongozi wakubwa, walitambua neema ile niliyojaliwa na Mungu wakatupatia mukono, mimi na Barnaba kuwa kitambulisho cha ushirika. Hivi tukapatana kwamba sisi tutakwenda kuhubiri watu wa mataifa mengine na wao watakwenda kuhubiri Wayuda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ