Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.
Atatangulia mbele ya kufika kwa Bwana, akiwa na roho na uwezo kama nabii Elia, kwa kuwapatanisha tena baba na watoto wao, na kuwageuza waasi wapate kuwa na hekima kama vile wenye haki. Hivi atamutayarishia Bwana watu wanaokuwa tayari kwa kumupokea.”
Mimi sikumujua ni nani, lakini yule aliyenituma kubatiza kwa maji aliniambia: ‘Yule utakayemwona Roho akishuka juu yake na kukaa juu yake, mutu yule ndiye anayebatiza kwa Roho Mutakatifu.’
Paulo akawaambia: “Yoane aliwabatiza wale waliogeuka toka zambi zao na kuwaambia Waisraeli kwamba wamwamini yule atakayekuja nyuma yake, naye ndiye Yesu.”