Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Lakini wamoja waliomupokea, ndio wale waliomwamini, aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 1:12
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata umewaimarisha watu wako Waisraeli kwa ajili yako mwenyewe, kusudi wakuwe watu wako milele; nawe ee Yawe umekuwa Mungu wao.


nitamupatia nafasi ya ukumbusho na ya sifa katika nyumba yangu na kuta zangu, nafasi bora kuliko kuwa na wana na wabinti. Nitamupatia jina la kukumbukwa siku zote na ambalo halitafutwa hata kidogo.


Yawe anasema: Wewe Israeli, mimi niliwaza hivi: heri ningekuhesabia kati ya wana wangu, na kukupa inchi nzuri ajabu, ndio urizi unaopita inchi zote za mataifa. Nilizani utaniita Baba Yako, na kwamba haungeacha kunifuata.


“Mutu anayewapokea ninyi, ananipokea mimi; naye anayenipokea, anamupokea yule aliyenituma.


Naye anayemupokea mutoto mudogo kama huyu kwa ajili ya jina langu, ananipokea mimi.


Alikuja katika inchi yake, lakini taifa lake halikumupokea.


Alikuja kushuhudia ule mwangaza kusudi watu wote wapate kuamini kwa njia yake.


Na kufa kwake si kwa ajili ya taifa hili tu, lakini vilevile kwa ajili ya watoto wa Mungu waliosambazwa, kusudi apate kuwaunga katika umoja.)


Wakati ule Yesu alipokuwa Yerusalema kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini kwa sababu waliona vitambulisho alivyofanya.


Lakini hii imeandikwa kusudi mupate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mupate uzima katika jina lake.


Anayemwamini Mwana hahukumiwi, lakini asiyemwamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.


Mutu huyu munayemujua na kumwona amepata tena nguvu kwa uwezo wa jina la Yesu, kwa njia ya kuaminia jina hili. Yeye amepona kabisa sawa vile ninyi wote munavyojionea, kwa njia ya kumwaminia Yesu.


Wote wanaoishi chini ya uongozi wa Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.


Roho huyo mwenyewe anahakikisha ndani ya roho zetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu.


Viumbe vyote vinangojea kwa hamu sana wakati Mungu atakapowaonyesha watoto wake waziwazi.


Kwa maana ninyi wote mumekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani na kuungana na Yesu Kristo.


Mungu alituma Roho wa Mwana wake ndani ya moyo wetu kwa kuhakikisha ya kuwa ninyi ni wana wake. Roho anayetuombea, akiita: “Baba!”


Basi kwa sababu mumemukubali Kristo kuwa Bwana wenu, muishi katika kuungana naye.


Kufuatana na hayo, ametupatia ahadi nzuri sana na kubwa mupate kuepuka uharibifu unaoletwa na tamaa mbaya za dunia na kushika hali yake ya kimungu.


Muangalie namna Baba alivyoonyesha upendo wake kwetu hata tupate kuitwa watoto wa Mungu! Na kwa hakika sisi ndio wao! Ndiyo maana watu wa dunia hawatutambui, kwa sababu hawakumujua Mungu.


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Wapendwa wangu, sasa sisi ni watoto wa Mungu, wala namna tutakavyokuwa haijaonekana bado waziwazi. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwa sababu tutamwona vile anavyokuwa.


Amri yake ndiyo hii tuamini jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane sisi kwa sisi kama vile Kristo alivyotuamuru.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ