Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 9:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Nitalia na kuomboleza juu ya milima; nitaomboleza juu ya mashamba ya nyama katika jangwa, kwa sababu yamekauka kabisa, hakuna mutu anayepita pahali pale. Hakusikiliki tena sauti za ngombe; ndege na nyama wamekimbia na kutoweka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 9:9
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–


Mutafanya nini siku ya azabu, siku zoruba itakapowakujia kutoka mbali? Mutamukimbilia nani kwa kuomba musaada? Mutakwenda wapi kwa kuweka mali yenu?


Munachagua mawe laini katika mabonde, na kuyafanya kuwa mungu wenu. Munayamwangia sadaka ya kinywaji na kuyapelekea sadaka ya unga! Mimi nitatulizwa kwa vitu hivyo?


Wamelifanya kuwa tupu; nalo linalilia katika ukiwa wake. Inchi yote imekuwa jangwa, wala hakuna mutu anayejali.


Mpaka wakati gani inchi itaomboleza kwa kukauka, na nyasi za mashamba yote kunyauka? Nyama na ndege wanakufa kwa uovu wa wakaaji wake. Wao wanasema: Mungu hataona mwisho wetu.


Niliangalia wala sikuona mutu; hata ndege katika anga walikuwa wametoweka.


Mimi sitawaazibu kwa ajili ya mambo haya? Nitaachilia taifa hili bila kulilipiza kisasi? –Ni ujumbe wa Yawe.


Basi, nisiwaazibu kwa ajili ya mambo haya yote? –Ni ujumbe wa Yawe.– Nisilipize kisasi juu ya taifa kama hili?


Kwa hiyo, inchi yote inakauka, wakaaji wake wote wanaangamia pamoja na nyama na ndege; hata samaki wanaangamizwa.


Ninakulilia wewe, ee Yawe, moto umemaliza malisho katika mbuga, ndimi za moto zimeteketeza miti katika mashamba.


Musikilize maombolezo yangu juu yenu, enyi Waisraeli:


Umeanguka na hautainuka tena ewe binti Israeli! Umeachwa ukiwa katika inchi yako, hakuna hata mutu wa kukuinua.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ