Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 9:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Wanalundika matendo ya kuzulumu juu ya mengine, nao udanganyifu juu ya udanganyifu. Wanakataa kunitambua mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.–

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 9:5
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha wakawapiga kwa kuwapofusha macho wanaume wote waliokuwa kwa mulango, wakubwa na wadogo, hata wakataabika kwa kutafuta ule mulango, nao hawakuupata.


Kupapayuka kwako kutanyamazisha watu? Kama ukichekelea watu, hakuna atakayekupatisha haya?


Uovu wako ndio unaongoza kinywa chako, nawe unachagua kusema kama wadanganyifu.


Watu hao wanafikiri mabaya siku zote, wanaamusha ugomvi kila mara.


Uko tayari siku zote kusema mabaya; kazi ya ulimi wako ni kutunga uongo.


Mbona, ewe jitu, unajivunia mabaya unayotendea waaminifu.


Unikinge na shauri baya la waovu, nayo fujo ya watu wabaya.


Atatayarisha silaha zake za hatari, na kuitia mishale yake moto.


Mawazo ya mwenye haki ni ya haki; mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.


Waovu hawalali hata kidogo wasipotenda uovu; hawapati usingizi wasipomukwaza mutu.


Ole kwao wanaokokota uovu kama kwa kamba; wanaoburura zambi kama wanavyokokota gari.


Mulichoka na safari zenu ndefu, hata hivyo hamukukata tamaa; mulijipatia nguvu mupya, ndiyo maana hamukuzimia.


Walipanda ngano, lakini walivuna magugu; wamejichokesha kwa bure. Kwa sababu ya hasira kali ya Yawe, watasikia haya juu ya mavuno yao.


Hata wandugu zako, jamaa yako mwenyewe, nao vilevile wanakudaganya; wanakukaripia waziwazi. Usiwaamini hata kidogo, ingawa wanakuambia maneno mazuri.


Mwetiopia anaweza kubadilisha rangi yake, au chui madoadoa yake? Nanyi muliozoea kufanya mabaya, munaweza namna gani kutenda mema?


Yawe anasema: Watu wangu ni wapumbafu, hawanijui mimi. Wao ni watoto wajinga; hawana ufahamu. Wao wanaelewa vizuri kutenda maovu, lakini hawajui kutenda mema.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Ukuta mukubwa wa Babeli utabomolewa mpaka chini, na milango yake mirefu itateketezwa kwa moto. Watu wanafanya juhudi za bure, mataifa yanajichokesha, maana mwisho wao ni katika moto!


Hivi ndivyo Babeli utakavyozama, wala hautainuka tena, kwa sababu ya hasara ambayo Yawe anauletea. Huu ndio mwisho wa maneno ya Yeremia.


Basi utawaambia: Ninyi ni taifa ambalo halikutii sauti ya Yawe, Mungu wao, wala kukubali maonyo yake. Kwenu uaminifu umekufa; umetoweka kabisa katika vinywa vyenu.


Kila mutu ajiepushe na jirani yake, wala asimwaminie ndugu yake! Maana ndugu ni mudanganyifu na kila jirani ni musingiziaji.


Nisiwaazibu kwa sababu ya mambo haya? –Ni ujumbe wa Yawe.– Nisililipize kisasi taifa kama hili?


Lakini ni kujisumbua bure; kutu yake nene haitoki hata kwa moto.


Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa, wakaaji wake wanasema uongo, kila neno wanalosema ni udanganyifu.


Anasema hivi: Enyi watu wangu, nimewatendea nini? Nimewachokesha kwa kitu gani? Munijibu!


Yawe wa majeshi anasababisha juhudi za watu zipotelee katika moto, na mataifa yajishugulishe bure.


Sisi wote si watoto wa baba mumoja? Sisi wote hatukuumbwa na Mungu yuleyule? Mbona basi, hatuaminiani sisi kwa sisi, na tunalizarau agano Yawe alilofanya na babu zetu?


Kwa hivi, muache uongo! Kila mumoja aseme ukweli kwa mwenzake, kwa maana sisi wote ni viungo vya mwili mumoja.


Wanadanganywa na watu wenye uongo na wanafiki wenye zamiri iliyokufa, iliyoharibika kabisa kama vile imeteketezwa kwa moto.


Kisha watu wote wa kizazi chake wakakufa, kizazi kingine kikafuata ambacho hakikumujua Yawe wala matendo aliyowatendea watu wa Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ