Kisha wakawapiga kwa kuwapofusha macho wanaume wote waliokuwa kwa mulango, wakubwa na wadogo, hata wakataabika kwa kutafuta ule mulango, nao hawakuupata.
Yawe anasema: Watu wangu ni wapumbafu, hawanijui mimi. Wao ni watoto wajinga; hawana ufahamu. Wao wanaelewa vizuri kutenda maovu, lakini hawajui kutenda mema.
Yawe wa majeshi anasema hivi: Ukuta mukubwa wa Babeli utabomolewa mpaka chini, na milango yake mirefu itateketezwa kwa moto. Watu wanafanya juhudi za bure, mataifa yanajichokesha, maana mwisho wao ni katika moto!
Basi utawaambia: Ninyi ni taifa ambalo halikutii sauti ya Yawe, Mungu wao, wala kukubali maonyo yake. Kwenu uaminifu umekufa; umetoweka kabisa katika vinywa vyenu.
Sisi wote si watoto wa baba mumoja? Sisi wote hatukuumbwa na Mungu yuleyule? Mbona basi, hatuaminiani sisi kwa sisi, na tunalizarau agano Yawe alilofanya na babu zetu?