Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 9:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kila mutu anadanganya jirani yake, hakuna hata mumoja anayesema ukweli. Wamezifundisha ndimi zao kusema uongo; anatenda uovu kwa kadiri ya kushindwa kabisa kunigeukia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 9:4
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye akamwuliza: “Jina lako nani?” Yeye akamujibu: “Yakobo.”


Nitateketeza yule anayemuteta mwenzake, sitamuvumilia mwenye majivuno na kiburi.


Anayemuchukia mwingine kwa siri ni munafiki. Anayemusingizia mutu ni mupumbafu.


Mutu anayetoa ushuhuda wa uongo juu ya mwenzake, ni hatari kama nyundo, upanga au mushale mukali.


Waovu hawalali hata kidogo wasipotenda uovu; hawapati usingizi wasipomukwaza mutu.


Maana uovu ndicho chakula chao, mateso makali ndiyo divai yao.


Kuna vitu sita Yawe anavyochukia, hata saba ambavyo ni chukizo kwake:


mushuhuda wa uongo anayesema uongo, na mutu anayechochea fitina kati ya wandugu.


Tumekuasi na kukukana, ee Yawe, tumekataa kukufuata, ewe Mungu wetu. Tunasema maneno ya kutesa na uasi, katika mioyo yetu tunatunga na kutoa maneno ya uongo.


Kwa hiyo, Yawe hawahurumii vijana wao, hana huruma juu ya wayatima na wajane wao; maana hakuna hata mumoja anayemufuata, kila mutu anasema upumbafu. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Hata wandugu zako, jamaa yako mwenyewe, nao vilevile wanakudaganya; wanakukaripia waziwazi. Usiwaamini hata kidogo, ingawa wanakuambia maneno mazuri.


Wote ni waasi na wagumu, ni watu wanaopitapita wakisengenya wengine, ni wagumu kama shaba au chuma. Wote wanatenda mabaya.


Nisiwaazibu kwa sababu ya mambo haya? –Ni ujumbe wa Yawe.– Nisililipize kisasi taifa kama hili?


Kwako kuna wanaowasingizia wengine kusudi wauawe. Wakaaji wako wanashiriki chakula kilichotolewa kwa miungu juu ya milima. Watu wako wanatenda uasherati.


Usipitepite hata kidogo ukiwachongea watu wa jamaa yako. Usitie maisha ya mwenzako katika hatari ya kifo kwa maneno yako. Mimi ni Yawe.


Sisi wote si watoto wa baba mumoja? Sisi wote hatukuumbwa na Mungu yuleyule? Mbona basi, hatuaminiani sisi kwa sisi, na tunalizarau agano Yawe alilofanya na babu zetu?


Mujilinde, kwa maana watu watawapeleka mbele ya tribinali kubwa nao watawapiga fimbo ndani ya nyumba zao za kuabudia.


“Ndugu atamutoa ndugu, kusudi auawe, na baba atamutoa mutoto wake, nao watoto watawageukia wazazi wao na kuwaua.


Mutatolewa hata na wazazi wenu, wandugu zenu, na watu wa jamaa zenu pamoja na warafiki zenu. Nao watawaua wamoja kati yenu.


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ