Yeremia 9:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
2 Ndimi zao ni hatari kama pinde; wameimarika kwa ajili ya uongo na si kwa ajili ya haki. Wanaendelea kutenda uovu kisha uovu, wala hawanitambui mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Ee Yawe, wewe ni mwenye haki, ingawa nitakushitaki. Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki: Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao? Mbona wote wanaodanganya wanastawi?
Nawe utajiuliza hivi katika moyo wako: Kwa nini mambo haya yamenipata? Sawa! Ikiwa kanzu yako imepandishwa, na kutendewa kwa kinguvu, hayo ni matokeo ya makosa yako mengi sana.
Maana, inchi imejaa wazinzi. Kwa sababu ya laana, inchi inaomboleza, na mashamba ya kulishia nyama yamekauka. Mienendo ya watu ni miovu, wanapoteza nguvu kwa ajili ya mambo yasiokuwa ya haki.
Yawe anasema: Watu wangu ni wapumbafu, hawanijui mimi. Wao ni watoto wajinga; hawana ufahamu. Wao wanaelewa vizuri kutenda maovu, lakini hawajui kutenda mema.
Mukimbie huko na huko katika Yerusalema, mupeleleze na kujionea wenyewe, muchunguze katika masoko yake. Mukiona hata mutu mumoja anayefuata sheria, mutu anayetafuta ukweli, basi Yawe atausamehe Yerusalema.
Watu wa Yuda wamekosa uaminifu kwa Mungu na kutenda machukizo katika Israeli na katika Yerusalema. Wamechafua hekalu la Yawe analolipenda. Tena wameoa wanawake wanaoabudu miungu ya kigeni.
Munauliza: Mbona sasa hazikubali? Yawe hazikubali kwa sababu anajua wazi kwamba umeivunja ahadi yako kwa muke wa ujana wako. Umekosa uaminifu kwake ingawa uliahidi mbele ya Mungu kwamba ungekuwa mwaminifu kwake.
Ninyi watu wasiokuwa na uaminifu! Hamujui kwamba kupenda raha ya dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi yeye anayetaka kupenda raha za dunia anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.