Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 8:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Mbona basi, watu hawa wameacha njia inayokuwa sawa na kuendelea katika upotovu wao? Wanashikamana na miungu yao ya uongo, na kukataa kunirudilia mimi!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 8:5
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Shika mafundisho ya hekima na usimwache iponyoke, uishike kwa uangalifu maana ni uzima wako.


Lakini mukikataa na kuniasi, mutaangamizwa kwa upanga. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Wanawaambia wale wanaopata maono hivi: Musipate maono. Wanawaambia manabii hivi: Musitutangazie ukweli, lakini mutuambie mambo ya kupendeza, mutoe unabii wa mambo ya udanganyifu tu.


Hapana! Mawazo yao yameambatana na hicho ambacho ni majivu tu! Mutu huyo amepotoka hata hawezi kujiokoa mwenyewe na kusema: Kweli, hiki ninachokuwa nacho katika mukono wangu ni udanganyifu mutupu!


Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.


Kijana binti anaweza kusahau mapambo yake, au bibi arusi nguo yake? Lakini watu wangu wamenisahau kwa muda wa siku zisizohesabika.


Utanikasirikia siku zote? Utachukizwa nami milele? Israeli, vile ndivyo unavyosema; na kumbe umetenda uovu wote ulioweza.


Kama vile kikapu kinachojaa ndege walionaswa, ndivyo nyumba zao zinavyojaa mali za udanganyifu. Ndiyo maana wamekuwa watu wakubwa na watajiri,


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Kwa hiyo simba kutoka pori atawaua; imbwa wa pori kutoka jangwa atawararua. Chui anaivizia miji yao. Kila mutu anayetoka humo atararuliwa vipandevipande, kwa sababu zambi zao ni nyingi, maasi yao ni makubwa.


Kisha nikawawekea walinzi kwa kuwaarifu nikawaambia: Musikilize mulio wa baragamu. Lakini wao wakasema: Hatutausikiliza.


Sikiliza, ee dunia! Mimi nitawaletea watu hawa hasara kulingana na nia zao mbaya. Maana hawakuyajali maneno yangu, na mafundisho yangu nayo wameyakataa.


Kwa hiyo, Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitawasafisha na kuwapima kwa moto kama vile chuma. Ni namna gani zaidi ya kuwatendea hawa watu wangu waovu?


Waisraeli wote wameiasi sheria yako, wamekuacha wakakataa kukutii. Kwa sababu tumekukosea, tumemwangiwa laana na viapo vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, mutumishi wako.


Basi, watarudi katika inchi ya Misri; watatawaliwa na mufalme wa Asuria, kwa sababu wamekataa kunirudilia.


Watu wangu wamekusudia kuniacha mimi, wakiitwa kusimama wapande juu, hakuna hata mumoja anayeweza.


Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!


Waisraeli ni wenye kichwa kigumu kama punda. Kwa nini basi Mungu ashugulike na kuwachunga, kama kondoo katika shamba kubwa la kuwakulishia?


Lakini watu walikataa kunisikiliza, waligeuza mabega na kuziba masikio yao kusudi wasisikie.


lakini ninyi hamutaki kuja kwangu mupate uzima.


Lakini muchunguze kila jambo na kushika lile linalokuwa jema.


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Lakini ninawaomba tu mushikamane na kile munachokuwa nacho mpaka nitakapokuja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ