Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 8:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Watu wote watakaobaki wa jamaa hii mbaya, pahali popote pale nilipowasambaza, wataona heri kufa kuliko kuishi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 8:3
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

naye akatembea mwendo wa siku nzima kuingia katika jangwa. Basi, akafika, akaikaa chini ya muti mumoja wa muretemu. Halafu, akaomba apate kufa, akisema: “Inatosha! Siwezi tena. Ee Yawe, sasa utoe uzima wangu. Mimi si bora kuliko babu zangu.”


Kisha, nitawakusanya kondoo wangu waliobaki kutoka inchi zote nilipowafukuza, na kuwarudisha katika malisho yao. Nao watazaa na kuongezeka.


Lakini wataapa wakisema: Kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyewaondoa na kuwaongoza Waisraeli kutoka inchi ya kaskazini na kutoka inchi zote ambapo alipowafukuza. Na halafu wataishi katika inchi yao wenyewe. –Ni ujumbe wa Yawe.


mutaniona. Nitatengeneza upya maisha yenu na kuwakusanya kutoka mataifa yote na pahali pote nilipowasambaza. Nitawarudisha pahali nilipowaondoa wakati nilipowapeleka katika uhamisho. –Ni ujumbe wa Yawe.


Maana yeye alituma habari huko Babeli, akisema: Mutabaki katika uhamisho kwa muda murefu, mujenge nyumba za kukalia, mulime mashamba, mupande mbegu na kula mazao yake!


wote walirudi kutoka pahali pote walipokuwa wametawanyika na kwenda katika inchi ya Yuda kwa Gedalia kule Misipa. Walichuma zabibu na matunda mengine kwa wingi sana.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninyi mumeona hasara yote niliyouletea Yerusalema na miji yote ya Yuda. Miji hii ni mabomoko mpaka leo wala hakuna mutu anayeishi humo.


Kwa hiyo, kasirani yangu na hasira yangu iliwaka na kumwangika juu ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalema, hata kukakuwa jangwa na mabomoko kama inavyokuwa mpaka leo.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Muwakusanye watu wote wa Israeli waliobaki kama vile watu wanavyookotesha zabibu katika shamba; kama vile muchumaji wa zabibu, mupitishe mikono katikati ya matawi yote.


Kwako, ee Bwana, kuna haki, lakini sisi tumepata haya siku zote. Jambo hili ni kweli kwetu sisi wote tunaoishi Yudea, wakaaji wa muji Yerusalema na Waisraeli wote ambao umewatawanya katika inchi za mbali na za karibu kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako.


Nitawatawanya ninyi kati ya watu wa mataifa na kuchomoa upanga juu yenu. Inchi yenu itakuwa ni ukiwa na miji yenu uharibifu.


Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:


Basi, sasa ee Yawe, ninakusihi uniondoe uzima wangu, maana ni vizuri kwangu kufa kuliko kuishi.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninapanga kuwaletea ninyi hasara, ambayo hamutaweza kuiponyoka hata kidogo. Utakuwa wakati mubaya kwenu, wala hamutaweza kutembea kwa maringo.


Musa akaendelea kusema: “Baraka na laana hizi zote zitatimizwa. Mutafikiri juu ya mambo hayo wakati Yawe, Mungu wenu, atakuwa amewatawanya kati ya mataifa.


Na hata kama mumetawanywa katika sehemu mbali kabisa katika dunia, Yawe, Mungu wenu, atawakusanya na kuwarudisha,


Nao wakaiambia milima na mawe: “Mutuangukie na kutufunika mbali na yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme na mbali na kasirani ya Mwana-Kondoo.


Na kwa muda ule, watu watatafuta kifo, lakini hakitawapata. Watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ