Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 7:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Musiwatese wageni, wayatima au wajane au kuwaua watu wasiokuwa na kosa katika inchi hii. Musijiangamize wenyewe kwa kuabudu miungu mingine.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 7:6
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye alimutoa mwana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Alipiga ramuli; aliaguza akishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


na kwa sababu ya damu isiyokuwa na kosa aliyoimwanga. Yawe hakumusamehe makosa hayo.


Walimwanga damu ya wasiokuwa na kosa, damu ya watoto wao wanaume na wabinti ambao waliwatoa sadaka kwa sanamu za Wakanana, nayo inchi ikachafuliwa kwa uuaji huo.


Usiondoe kitambulisho cha mupaka wa zamani, wala usinyanganye mashamba ya wayatima,


Muko mbio kutenda maovu, muko wepesi kumwanga damu isiyokuwa na kosa. Mawazo yenu ni mawazo ya uovu, popote munapokwenda munaacha ukiwa na uharibifu.


Watu hawa waovu wanakataa kusikia maneno yangu. Wanaendelea na kufuata mawazo yao wenyewe. Wanaifuata miungu mingine, wanaitumikia na kuiabudu. Hao watakuwa kama mukaba huu ambao haufai kitu.


Kwa maana watu wameniacha mimi na kuchafua nafasi hii kwa kufukizia miungu mingine ubani; miungu ambayo wao wenyewe, babu zao wala wafalme wa Yuda hawaijui. Zaidi ya ile wamejaza pahali hapa damu ya watu wasiokuwa na kosa,


Niliwaazibu ninyi lakini ilikuwa bure, ninyi munakataa maonyo. Muliwateketeza manabii wenu kwa upanga kama simba mwenye uchu.


Juu ya nguo zako kuna damu ya wamasikini wasiokuwa na kosa, ijapokuwa haukuwakuta wakivunja nyumba yako. Na zaidi ya hayo yote,


Lakini mujue kwa hakika kwamba mukiniua, mutakuwa mumejiletea laana ninyi wenyewe kwa kumwanga damu isiyokuwa na kosa, na kuleta laana juu ya muji huu na wakaaji wake. Maana, ni kweli kwamba Yawe alinituma niwaambie mambo hayo kusudi muyasikie.


Wao wakamurudisha Uria kutoka Misri, wakamupeleka kwa mufalme Yoyakimu. Mufalme akamwua kwa upanga na maiti yake ikatupwa katika kaburi.


Niliwapelekea tena na tena watumishi wangu wote, ni kusema manabii wawaambie kila mumoja wenu aachane na mwenendo wake mwovu, abadilishe matendo yake na kuacha kuifuata na kuitumikia miungu mingine. Na kwamba mukifanya hivyo mutakaa katika inchi niliyowapa ninyi na babu zenu. Lakini ninyi hamukunitegea sikio wala hamukunisikiliza.


wamenenepa na kungaa vizuri. Maovu yao hayana mwisho, hawahukumu yatima kwa kufuatana na sheria kusudi wapate kufanikiwa, wala hawatetei haki za watu wakosefu.


Lakini mugeuze mwenendo wenu na matendo yenu. Mufuate sheria yangu kati yenu.


Munaiba, munaua, munafanya uzinzi, munaapa kwa uongo, munamufukizia mungu Bali ubani na kuabudu miungu mingine ambayo hamujapata kuijua.


Ni kwa sababu ya zambi za manabii wake na makosa ya makuhani wake, ambao walimwanga damu ya watu wa haki katika muji wake.


Kwako baba na mama wanazarauliwa. Mugeni anayekaa kwako ananyanganywa mali yake. Wayatima na wajane wanaonewa.


Kama kuna mugeni katika inchi yako usimutendee vibaya.


Musipunjane, lakini, mutamwogopa Mungu wenu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Nao watu wote wakajibu: “Lazima ya damu ya mutu huyu ikuwe juu ya kichwa chetu na juu ya kichwa cha watoto wetu!”


Akawaambia: “Nimekosa kwa kumutoa mutu huyu asiyekuwa na kosa auawe.” Lakini wao wakamujibu: “Jambo hilo halituelekei. Ni kazi yako wewe mwenyewe!”


na laana, kama hamutatii amri za Yawe, Mungu wenu, na kuacha njia ninayowaamuru, mukiabudu miungu mingine ambayo hata hamujajua bado.


“Musipotoshe haki za wageni na wayatima. Wala musitwae nguo ya mujane kuwa rehani.


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayepotosha haki ya mugeni au yatima au mujane’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


Lakini mukimusahau Yawe, Mungu wenu, na kufuata miungu mingine kwa kuitumikia na kuiabudu, ninawaonya vikali leo hii kwamba hakika mutaangamia.


Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ