Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 7:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Inchi itakuwa jangwa na katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalema nitakomesha sauti zote za furaha na shangwe, nazo nyimbo za wenye kufanya ndoa, kwa sababu inchi itakuwa ukiwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 7:34
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Usiku ule ukuwe tasa, sauti ya furaha isiingie ndani yake.


Moto ukawateketeza vijana wao wanaume, na wabinti wao wakakosa wachumba.


Inchi yenu imeharibiwa kabisa; miji yenu imeteketezwa kwa moto. Wageni wamebeba mazao ya inchi yenu mbele ya macho yenu, imeharibiwa kama vile Sodoma.


Halafu watu watalia na kuomboleza kwenye milango ya muji; nao wataikaa ndani ya mavumbi katika ukiwa.


Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.


Maana Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nitazikomesha kabisa kutoka pahali hapa sauti za furaha na shangwe, nazo nyimbo za wenye kufanya ndoa. Nitayafanya hayo yote katika nyakati zenu, na mutayaona waziwazi.


Yawe anasema hivi juu ya nyumba ya kifalme ya Yuda: Ingawa unaonekana vizuri kama inchi ya Gileadi, kama vichwa vya milima ya Lebanoni, ninaapa kwamba nitakufanya kuwa jangwa, ukuwe muji usiokaliwa na watu.


Tena, nitakomesha toka kati yao sauti za furaha, sauti za wenye kufanya ndoa, wala sauti za kusaga hazitasikilika, wala mwangaza wa taa hautaonekana.


Musiwasikilize. Mumutumikie mufalme wa Babeli, kusudi mupate kuishi. Kwa nini muji huu ufanywe kuwa mabomoko?


Yawe anasema hivi: Katika muji huu ambao munasema kwamba umekuwa ukiwa bila watu wala nyama, katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema ambazo ni tupu, bila watu wala nyama, humo kutasikilika tena sauti za vicheko, sauti za furaha,


sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Niliona inchi yote yenye mboleo imegeuka jangwa, nayo miji yake yote imebaki mabomoko matupu, kwa sababu ya hasira kali ya Yawe.


Maana Yawe anasema hivi: Inchi nzima itakuwa jangwa tupu; lakini sitaiharibu kabisa.


Kwa hiyo, kasirani yangu na hasira yangu iliwaka na kumwangika juu ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalema, hata kukakuwa jangwa na mabomoko kama inavyokuwa mpaka leo.


Wazee wameacha kutoa mashauri yao, vijana wameacha kuimba.


Nitakomesha muziki wa nyimbo zako. Sauti za vinubi vyako hazitasikilika tena.


Mateso makali yanaendelea kuwa mubaya zaidi. Hakuna hata mumoja kati yenu atakayebaki, wala vitu mulivyojilundikia kwa wingi au utajiri wenu; hakutakuwa mutu mwenye heshima kati yenu.


Kwa hiyo wakati wa mavuno nitaitwaa ngano yangu, nitaiondoa divai yangu kwa wakati wake. Nitamunyanganya nguo zangu za sufu na kitani, ambazo zilitumika kuufunika uchi wake.


Nitakomesha furaha zake zote, sikukuu zake za mwandamo wa mwezi na za Sabato, na sikukuu zote zilizoamriwa.


Nitawatawanya ninyi kati ya watu wa mataifa na kuchomoa upanga juu yenu. Inchi yenu itakuwa ni ukiwa na miji yenu uharibifu.


Lakini inchi yote nyingine itakuwa jangwa, kwa sababu ya uovu wa wakaaji wake.


Mwangaza wa taa hautaonekana tena ndani yako. Na hakutasikilika tena kelele la wenye kuoa au kuolewa. Itakutokea vile kwa sababu wachuuzi wako walikuwa wenye uwezo mukubwa katika dunia, nawe umewadanganya watu wote kwa njia ya vitendo vyako vya uchawi.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ