Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 7:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Lakini niliwapa amri kwamba waitii sauti yangu kusudi nikuwe Mungu wao, nao wakuwe watu wangu. Niliwaamuru vilevile waishi kama nilivyowaagiza, kusudi wapate uheri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 7:23
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakimutii Mungu na kumutumikia, wanafanikiwa katika siku zao zote; miaka yao yote inakuwa ya furaha.


watu wasiotenda uovu hata kidogo, lakini wanafuata siku zote njia zake.


Ee Yawe, Mungu wangu, umetufanyia maajabu mengi, na mipango yako juu yetu haihesabiki; hakuna yeyote anayekuwa kama wewe. Kama ningeweza kusimulia hayo yote, hesabu yake ingenishinda.


Hivyo, nikawaacha wabaki katika ugumu; wafuate mashauri yao wenyewe.


akawaambia: “Ikiwa mutaisikiliza kwa uaminifu sauti yangu mimi Yawe, Mungu wenu, kutenda yale yanayokuwa sawa mbele yangu, na kuheshimu amri na masharti yangu yote, basi, mimi sitawaletea yale magonjwa niliyowaletea Wamisri. Kwa sababu, mimi ni Yawe ninayewaponya ninyi.”


Musa akawaambia: “Hili ndilo agizo la Yawe: Mutwae kipimo kimoja cha litre ine ya mana na kukiweka kwa ajili ya wazao wenu, kusudi waweze kuona chakula nilichowakulisha katika jangwa wakati nilipowatoa katika inchi ya Misri.”


Muwaambie watu wa haki jinsi wanavyokuwa na heri, maana watakula matunda ya matendo yao.


Hili ni agano nililowaagiza babu zenu kutii nilipowaondoa katika inchi ya Misri, kutoka katika shimo la moto. Niliwaambia wanitii na kufanya yote niliyowaamuru, na kwamba wakifanya hivyo, watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.


Maana niliwaonya vikali babu zao nilipowaondoa katika inchi ya Misri, nami nimeendelea kuwaonya wanitii mpaka siku hii ya leo.


Kama vile mukaba unavyoshikamana na kiuno cha mutu, ndivyo nilivyowashikamanisha nami watu wa Israeli na watu wa Yuda, kusudi wajulikane kwa jina langu, wanisifu na kunitukuza. Lakini wao hawakunisikiliza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe aliongea nanyi mulipokuwa katika ustawi, lakini ninyi mukasema: Hatutasikiliza. Hii ndiyo tabia yenu tangu utoto wenu, hamujatii sauti ya Yawe.


Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki. Muokoe kila mutu aliyenyanganywa mali zake toka katika mikono ya mutesaji. Musiwatendee vibaya au kwa ukali wageni, wayatima na wajane, wala musimwange damu ya mutu asiyekuwa na kosa kwa nafasi hii.


Nitawapa moyo wa kujua kwamba mimi ndimi Yawe. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; maana watanirudilia kwa moyo wao wote.


Kisha siku hizo, nitafanya agano hili na Waisraeli. Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.


Yeremia akamujibu: Hautatolewa kwao. Wewe sasa utii kile Yawe anachosema, kama ninavyokuambia, na mambo yote yatakuendekea vema, na maisha yako yataokolewa.


Ikuwe ni jambo la kupendeza au hapana, sisi tutaitii sauti ya Yawe, Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake kusudi mambo yatuendekee vizuri tutakapomutii Yawe, Mungu wetu.


Hausikilizi onyo lolote, wala haukubali kutii. Haukumutegemea Yawe hata kidogo, wala kumukaribia Mungu wake.


Watu wanaokaa katika inchi za mbali watakuja kusaidia kwa kulijenga hekalu langu mimi Yawe. Nanyi mutajua kwamba Yawe wa majeshi, ndiye aliyenituma kwenu. Haya yote yatatukia kama mukiitii sauti ya Yawe, Mungu wenu.


Haya ndiyo mambo ambayo mimi Yawe niliyowaambia kupitia kwa manabii wa zamani, wakati Yerusalema ulikuwa umestawi na wenye wakaaji tele, na wakati ambapo kulikuwa wakaaji wengi katika miji ya kandokando yake na katika eneo la Negebu na mabonde ya Sefela.


Lakini sasa yamefunuliwa na maandiko ya manabii kufuatana na amri ya Mungu wa milele, kusudi mataifa yote yapate kumwamini na kumutii.


kuangusha vizuizo vyote watu wanavyojivunia kwa kupinga elimu ya Mungu. Tunatawala mafikiri ya watu na kuyafanya yapate kumutii Kristo.


baraka, kama mutatii amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa hivi leo;


musisikilize maneno ya nabii huyo au mutabiri wa kutumia ndoto, kwa maana Yawe, Mungu wenu, anawatumia kwa kuwajaribu kusudi ajue kama munamupenda yeye Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.


Mufuate na kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kushika amri zake na kutii sauti yake. Mumutumikie na kuambatana naye.


Mukimurudilia Yawe, Mungu wenu, ninyi na watoto wenu, mukitii kwa moyo wote na roho yote neno lake ninalowaamuru leo,


Mumupende Yawe, Mungu wenu. Muitii sauti yake na kuambatana naye. Kama munafanya hivyo, mutapata maisha marefu na kuishi katika inchi ambayo Yawe aliwaahidi wazee wenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo, kwamba atawapa.”


Nanyi mutatii sauti ya Yawe na kushika amri zake zote ninazowapa leo.


juu ya siku ile ambayo mulisimama mbele ya Yawe, Mungu wenu, kule Horebu, ndio Sinai, aliponiambia: ‘Muwakusanye hao watu mbele yangu, niwaambie maneno yangu kusudi wajifunze kuniogopa mimi siku zote za maisha yao, na kuwafundisha watoto wao kufanya hivyo’.


Kwa hiyo mushike masharti yake na amri zake ambazo ninawapa leo kusudi mufanikiwe, ninyi pamoja na wazao wenu, na kuishi siku nyingi katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa ikuwe yenu milele.”


“Uheshimu baba yako na mama yako, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru, kusudi uishi maisha marefu na kufanikiwa katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Heri wangekuwa siku zote na mawazo kama haya wakiniheshimu na kushika amri zangu! Mambo yao yote yangewaendekea vizuri, wao wenyewe na wazao wao milele.


Mutafuata njia yote Yawe, Mungu wenu, aliyowaamuru kufuata kusudi mambo yenu yawaendekee vizuri na mupate kuishi muda murefu katika inchi mutakayotwaa ikuwe mali yenu.


Kwa hiyo enyi Waisraeli, mukuwe waangalifu kwa kuzitimiza, kusudi mufanikiwe na kuongezeka sana katika inchi hiyo inayotiririka maziwa na asali kama vile alivyowaahidi.


Na alipokwisha kufanywa kuwa mukamilifu, akawaongoza watu wote wanaomutii wapate kuokolewa kwa milele.


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ