Yeremia 7:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200218 Watoto wanaokota kuni, wababa wanawakisha moto na wamama wanaponda unga kwa ajili ya kutengeneza mikate ya kumutambikia mungu wa kike, wanayemwita malkia wa mbinguni. Tena wananikasirikisha kwa kuitolea miungu mingine sadaka ya divai. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ninyi pamoja na wake wenu mumetimiza kwa vitendo yale muliyosema kwa vinywa vyenu, mukisema kwamba mumekusudia kutimiza viapo vyenu mulivyofanya vya kumutolea malkia wa mbinguni ubani na kumutolea sadaka ya kinywaji. Basi mushike viapo vyenu na kutoa sadaka za vinywaji!
Kisha akanipeleka mpaka katika uwanja wa ndani wa nyumba ya Yawe. Huko kwenye mulango wa hekalu, kati ya baraza na mazabahu, kulikuwa wanaume yapata makumi mbili na watano, wakigeuzia mugongo wao upande wa hekalu, na nyuso zao zikielekea upande wa mashariki. Walikuwa wanaabudu jua wakielekea upande wa mashariki.