Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 7:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Watoto wanaokota kuni, wababa wanawakisha moto na wamama wanaponda unga kwa ajili ya kutengeneza mikate ya kumutambikia mungu wa kike, wanayemwita malkia wa mbinguni. Tena wananikasirikisha kwa kuitolea miungu mingine sadaka ya divai.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 7:18
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe umetenda uovu mubaya zaidi kuliko waliotenda wale waliokutangulia. Wewe umenikasirikisha kwa kujitengenezea miungu mingine na sanamu za kufua, kisha umeniacha.


“Wewe Basha, mimi nilikuinua kutoka katika mavumbi, nikakufanya kiongozi wa watu wangu Waisraeli. Wewe umefuata mwenendo wa Yeroboamu. Uliwasukuma watu wangu Waisraeli watende zambi na kunikasirikisha kwa zambi zao.


Lakini wanaoabudu miungu mingine, watapata mateso mengi. Sitaitolea sadaka za damu hata kidogo, na majina ya miungu hiyo sitayataja.


Watu wa Yerusalema wamejikwaa, watu wa Yuda wameanguka, kwa sababu wanamupinga Yawe kwa maneno na matendo, wakizarau utukufu wake kati yao.


Munachagua mawe laini katika mabonde, na kuyafanya kuwa mungu wenu. Munayamwangia sadaka ya kinywaji na kuyapelekea sadaka ya unga! Mimi nitatulizwa kwa vitu hivyo?


Lakini nitafanya nini na ninyi munaoniacha mimi Yawe, musioujali Sayuni, mulima wangu mutakatifu, munaotolea miungu chakula na divai kusudi iwapatie bahati zuri.


Ni watu ambao wananichokoza waziwazi siku zote; wanatambikia miungu yao katika bustani, na kuifukizia ubani juu ya matofali.


Nami nitawahukumu Waisraeli kwa ajili ya uovu wao wote, kwa maana waliniacha mimi na kuifukizia miungu mingine ubani na kuabudu sanamu walizojitengenezea wenyewe.


Mimi Yawe wa majeshi niliuotesha huu muzeituni; lakini sasa ninatangaza hasara juu yake, kwa sababu ya maovu ambayo watu wa Israeli na Yuda wameyafanya. Wamenikasirikisha kwa kumufukizia mungu Bali ubani.


Watoto wao wanakumbuka mazabahu zao na sanamu za mungu muke, Ashera, zilizowekwa kando ya miti mibichi, juu ya vilele vya vilima


Nyumba za Yerusalema na nyumba za wafalme wa Yuda, ndizo nyumba zote ambazo juu ya paa zao watu walifukiza ubani kwa kutambikia makundi ya nyota, na kuitolea miungu mingine sadaka za divai, zote zitageuzwa kuwa chafu kama Tofeti.


Lakini mulikataa kunisikiliza. Na kisha, mulinikasirikisha na sanamu mulizojitengenezea wenyewe, na kwa hiyo mukajiletea hasara ninyi wenyewe. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wakaldea wanaoushambulia muji huu wataingia na kuuteketeza kwa moto; watauteketeza pamoja na nyumba ambazo juu ya paa zake ubani ulifukiziwa kwa mungu Bali na sadaka za divai zilitolewa kwa miungu mingine, kwa kunichokoza.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ninyi pamoja na wake wenu mumetimiza kwa vitendo yale muliyosema kwa vinywa vyenu, mukisema kwamba mumekusudia kutimiza viapo vyenu mulivyofanya vya kumutolea malkia wa mbinguni ubani na kumutolea sadaka ya kinywaji. Basi mushike viapo vyenu na kutoa sadaka za vinywaji!


Hata hivyo, mimi niliwatuma kwenu siku zote watumishi wangu manabii nikisema: Musifanye jambo hili baya ninalolichukia!


Wewe hauoni mambo wanayofanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema?


Vijana wanalazimishwa kusaga ngano kwa mawe, watoto wanayumbayumba kwa mizigo ya kuni.


Tena ulifanya uzinzi na jirani zako Wamisri waliojaa tamaa, ukaongeza uzinzi wako na kuichochea hasira yangu.


Maana nilipowapeleka katika ile inchi niliyoapa kuwapa, kila mara walipoona kilima kirefu au miti ya majani mengi, walianza kutoa matambiko na sadaka zao na kunichokoza. Kulekule walitoa sadaka za harufu nzuri na kutoa sadaka za kinywaji.


Kisha akanipeleka mpaka katika uwanja wa ndani wa nyumba ya Yawe. Huko kwenye mulango wa hekalu, kati ya baraza na mazabahu, kulikuwa wanaume yapata makumi mbili na watano, wakigeuzia mugongo wao upande wa hekalu, na nyuso zao zikielekea upande wa mashariki. Walikuwa wanaabudu jua wakielekea upande wa mashariki.


Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeyaona mambo hayo? Hata hivyo, watu wa Yuda wanaona machukizo hayo kuwa ni kidogo. Wanajaza mateso makali katika inchi na kuzidi kunikasirikisha. Angalia jinsi wananichukiza!


Au tunataka kumuchokoza Bwana hata asikie wivu? Munafikiri kuwa sisi tuko na nguvu kuliko yeye?


Wakamufanya aone wivu mukali kwa miungu yao, wakamuchochea akasirike kwa matendo yao ya kuchukiza.


Wamenichochea kuona wivu kwa kitu kisichokuwa mungu, wamenikasirikisha kwa sanamu zao. Hivyo nitawafanya waone wivu juu ya watu wa bure, nitawakasirikisha kwa kutumia taifa la wapumbafu.


Mufanye angalisho kusudi wakati mutakapoangalia na kuona nyota, vitu vyote vya mbinguni, musivutwe kuviabudu na kuvitumikia. Vitu hivyo Yawe amewaachia watu wengine waviabudu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ