Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 51:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Tulijaribu kuuponyesha Babeli, lakini hauwezi kupona. Muuache, tujiendee, kila mumoja katika inchi yake. Hukumu yake ni kubwa sana inafika mpaka katika mawingu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 51:9
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini kule Samaria kulikuwa nabii wa Yawe, jina lake Obedi. Yeye alitoka kwenda kukutana na waaskari wa Israeli walipokuwa karibu kuingia Samaria, akawaambia: “Yawe, Mungu wa babu zenu, alikuwa amewakasirikia watu wa Yuda, ndiyo maana aliwatia katika mikono yako lakini umewaua kwa hasira. Tendo hilo limetoka mbinguni.


nikisema: “Ee Mungu wangu, ninaona haya kubwa sana kukiinua kichwa changu mbele yako. Zambi zetu zimelundikana kupita hata vichwa vyetu; makosa yetu yanafika hata mbinguni.


Kama swala anayewindwa, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji, kila mumoja atajiunga na watu wake, kila mutu atakimbilia katika inchi yake.


Ndivyo watakavyokuwa hao uliowategemea hivyo, hao uliojishugulisha nao tangu ujana wako. Watatangatanga kila mumoja njia yake; hakuna hata mumoja atakayeweza kukuokoa.


Wengi walijikwaa, wakaanguka, kisha wakaambiana wao kwa wao: Musimame, tuwaendee watu wetu, turudi katika inchi yetu, tuukimbie upanga wa adui.


Hata waaskari wake wa mushahara ni kama wana-ngombe wanono; nao tena wamegeuka, wakakimbia pamoja, wala hawakuweza kuvumilia, kwa maana siku yao ya kuangamizwa imefika, wakati wao wa kuazibiwa umetimia.


Muzuie watu wasipande mbegu Babeli, wala wasivune wakati wa mavuno. Kutokana na upanga wa uharibifu, kila mumoja atawarudilia watu wake, kila mumoja atakimbilia katika inchi yake.


Wakati wa mavuno umepita, nao wakati wa jua kali umekwisha, nasi hatujaokolewa!


Ole kwao kwa sababu wameniacha! Maangamizi yawapate, maana wameniasi. Nilitaka kuwakomboa, lakini wanasema uongo juu yangu.


Kisha nikasikia sauti ingine kutoka mbinguni ikisema: “Mutoke katika muji ule ninyi watu wangu, kusudi musishiriki zambi zake na kupatwa vilevile na mapigo yatakayoupata.


Kwa maana zambi zake zinazidi sana hata zimefika mbinguni na Mungu hakusahau mabaya yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ