Angalia, wanakuja: waaskari wapanda-farasi wawiliwawili. Wanasema: Babeli umeanguka! Umeanguka! Sanamu zote za miungu yake zimetupwa chini na kuvunjwavunjwa!
Lakini hasara itakupata ambayo hautaweza kujiepusha nayo. Magumu yatakutokea ambayo hautaweza kuyapinga; maangamizi yatakufikia kwa rafla ambayo haujapata kuyaona hata kidogo.
Haya yote mawili yatakupata kwa rafla katika siku moja: kupoteza watoto wako na kuwa mujane, ijapokuwa una wingi wa uchawi wako, na nguvu nyingi za uganga wako.
Mutangaze kati ya mataifa, munyanyue bendera na kutangaza, musifiche jambo lolote. Museme: Babeli umetekwa, mungu Beli amepatishwa haya. Merodaki amefazaishwa; sanamu zake zimefezeheshwa, miungu yake imefazaishwa.
Malaika wa pili akafuata yule wa kwanza akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa, ule muji mukubwa Babeli. Umewakunywesha mataifa yote divai yake kali, ukiwalewesha na maovu ya uasherati wake.”
Halafu akalalamika kwa sauti kubwa, akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa ule muji mukubwa Babeli! Sasa umekuwa makao ya mashetani ya kila namna, ya pepo wachafu, na makimbilio ya ndege wote wachafu na wenye kuchukiza.