Yeremia 51:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Usiwape nafasi wapiga mushale wa Babeli; usiwaache wavute upinde, wala kuvaa nguo zao za vita. Usiwahurumie vijana wake; uangamize kabisa jeshi lake.
Enyi wafundi wote wapiga mishale, mujipange kwa kuzunguka muji wa Babeli kwa vita; mupige mishale, musiache mushale hata mumoja, maana umenikosea mimi Yawe.
Mupande, muiendee inchi ya Merataimu, muende kuishambulia; muwashambulie wakaaji wa Pekodi na kuwaangamiza kabisa watu wake. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mufanye kila kitu nilichowaamuru.
Sema: Huu ni ujumbe wa Yawe: Maiti za watu zinalala chini kila pahali kama malundo ya mboleo katika mashamba, kama miganda iliyoachwa na muvunaji, wala hakuna anayeikusanya.