Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 50:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kwa maana, taifa kutoka kaskazini limefika kuushambulia; litaifanya inchi yake kuwa uharibifu. Hakuna atakeyeishi humo; watu na nyama watakimbia mbali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 50:3
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

wanadamu, nyama, ndege na samaki. Vyote nitaviangamiza. Waovu nitawaangamiza kabisa; wanadamu nitawateketeza kabisa katika dunia.


Yawe amezichochea roho za wafalme wa Wamedi, kwa maana amekusudia kuiangamiza Babeli. Kweli, hicho ndicho kisasi cha Yawe; analipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake. Munoe mishale yenu! Mutwae ngao!


Kisha umalizie na maneno haya: Ee Yawe, wewe umesema kwamba utaharibu nafasi hii hata kusikaliwe na kiumbe chochote, mwanadamu au nyama, na kwamba inchi hii itakuwa jangwa milele.


Maana, mimi nitachochea mataifa makubwa kutoka inchi ya kaskazini washambulie inchi ya Babeli. Watajitayarisha kuishambulia inchi ya Babeli na kuiteka. Mishale yao ni kama shujaa hodari asiyerudi mikono mitupu.


Kisha mbingu, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yao vitaimba kwa furaha juu ya kuanguka kwa Babeli, wakati waangamizaji watakapofika kutoka upande wa kaskazini kuushambulia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nitawaua wakaaji wa muji huu: wanadamu na nyama vilevile. Watakufa kwa magonjwa makali sana.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaimwanga hasira yangu juu ya pahali hapa, juu ya wanadamu na nyama, miti katika mashamba na juu ya mazao ya inchi. Nayo nafasi hii itawaka moto wala hautaweza kuzimishwa.


“Usiku ule, nitapita katika inchi ya Misri na kuwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri, watu na nyama. Nitaiazibu miungu yote ya Misri. Mimi ni Yawe.


Hivyo akasema: “Nitamuharibu kabisa katika dunia mwanadamu niliyemwumba, pamoja na nyama wa pori, viumbe vinavyotambaa na ndege wa anga. Ninasikitika kwamba niliwaumba katika dunia.”


Nimetokeza mutu toka kaskazini, naye amekuja; nimemuchagua mutu toka mashariki, naye atalitaja jina langu. Yeye atawakanyaga wafalme kama matope, kama vile mufinyanzi anavyoponda udongo wake.


Yawe anasema hivi kwa Kiro, muchaguliwa wake: Nilikuchagua kuwa mufalme kwa kunitumikia. Ninaimarisha nguvu yako kusudi uyashinde mataifa mbele yako, na kuzivunja nguvu za wafalme. Mimi ninafungua milango ya muji mbele yako, na hakuna mulango utakaofungwa.


Yawe anasema: Nitaifanya Yerusalema kuwa mabomoko matupu, nitaifanya kuwa pango la mbweha; na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa, pahali pasipokaliwa na mutu yeyote.


Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ