Ewe Sayuni, kamba zako zimeregea, haziwezi kushikilia matanga yake, wala kufungia paa zao. Lakini vitu vingi vilivyonyanganywa vitagawanywa; hata vilema wataweza kupata sehemu yao.
Hiyo miaka makumi saba itakapopita, nitamwazibu mufalme wa Babeli pamoja na taifa lake. Nitaiangamiza inchi hiyo ya Wababeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitafanya hivyo kwa sababu ya uovu wao na kuifanya inchi ibaki mabomoko hata milele.
Mataifa yote yatamutumikia yeye, pamoja na mwana wake na mujukuu wake mpaka wakati inchi yake itakapoanguka. Kisha mataifa mengi na wafalme wengi wakubwa watamufanya kuwa mutumwa wao.
Mukuje kumushambulia kutoka kila upande; muzifungue gala zake za chakula; mumulundikie malundo ya ngano! Muiangamize kabisa inchi hii; musiache kitu chochote!
Upanga ukuwe juu ya farasi wake na magari yake, juu ya majeshi yake yote ya mushahara, kusudi wakuwe sawa na wanawake! Upanga ukuwe juu ya hazina zake zote kusudi zinyanganywe.
Watu wa Sayuni watasema: Babeli ulipizwe mateso makali yaleyale tuliyotendewa sisi pamoja na jamaa zetu! Yerusalema itasema: Damu yangu ikuwe juu ya wakaaji wa Kaledea.
Nikiwa katika maono hayo, Roho wa Mungu alininyanyua na kunipeleka mpaka katika inchi ya Babeli, kwa watu wanaokuwa kule katika uhamisho. Kisha maono hayo yakatoweka.
Wewe umenyanganya mataifa mengi, lakini wote wanaobaki watakunyanganya wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.
Zile pembe kumi ulizoona na yule nyama wa ajabu watamuchukia yule kahaba. Watamunyanganya vyote anavyokuwa navyo na kumwacha uchi. Nao watakula nyama ya mwili wake na kuteketeza mabaki yake kwa moto.