Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 5:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 5:3
45 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kesho yake, yule binti wa kwanza akamwambia yule mudogo: “Jana usiku mimi nililala na baba. Leo vilevile tumuleweshe kwa divai, kisha wewe utalala naye, na hivyo sisi wote tutadumisha uzao kwa kupata watoto.”


Yeroboamu hakuuacha upotovu wake; aliendelea kuchagua watu wa kawaida kuwa makuhani, watumike kwa nafasi ya kutambikia juu ya vilima. Mutu yeyote aliyejitolea, alimutakasa kuwa kuhani wa nafasi ya kutambikia kule juu ya vilima.


Kwa mara ingine tena, mufalme akatuma kiongozi mwingine na watu wake makumi tano. Kiongozi wa tatu akapanda kwenye mulima, akapiga magoti mbele ya Elia na kumusihi akisema: “Ewe mutu wa Mungu, ninakusihi uyahesabu maisha yangu na maisha ya hawa watumishi wako makumi tano yakuwe ya bei kali mbele yako.


Yawe anachunga kwa uangalifu ulimwengu wote, kwa kuwapa nguvu wale wanaokuwa waaminifu kwake. Umetenda jambo la kipumbafu, kwa hiyo tangu sasa, utakuwa na vita kila mara.”


Wakati alipokuwa katika taabu zaidi, mufalme huyu Ahazi alizidi kumwasi Yawe.


Nimekukosea wewe peke yako, nimetenda mabaya mbele yako. Hivi uamuzi wako ni wa haki, hukumu yako haipotoki.


Wewe unataka moyo wa ukweli; hivyo unifundishe kuwa na moyo wa hekima.


Mungu anayetawala tangu milele, atanisikia na kuwafezehesha waadui yangu, maana hawapendi kubadilika, wala hawamwogopi Mungu.


Mutu mwovu anajionyesha kuwa hodari, lakini mutu wa usawa anafikiri vizuri juu ya mwenendo wake.


Yawe analinda maarifa lakini anayavuruga maneno ya waovu.


Utasema: “Nimepigwa, lakini sikuumia; wamenipondaponda, lakini sikusikia kitu. Nitaamuka saa gani kusudi nitafute kinywaji kingine?”


Hata kama ukitwanga mupumbafu katika kinu, sawa na ngano, hautaweza kumutenganisha na upumbafu wake.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Kwa hiyo aliwamwangia kasirani yake kali, akawaacha kupatwa na vita kali. Hasira yake iliwawakia kila upande, lakini wao hawakuelewa chochote; iliwachoma, lakini hawakufikiri juu ya jambo hilo.


Lakini nilikujua wewe kuwa na moyo mugumu; kichwa kigumu kama chuma, uso wako kama shaba.


Yawe atakata katika Israeli kichwa na mukia, tawi la mingazi na nyasi, kwa muda wa siku moja tu.


Nimepepeta watu wangu kwa kuwasambaza sawa maganda, toka katika kila muji wa inchi yao. Nimewaangamiza kwa kuwaua watoto wao, lakini hawakuacha mwenendo wao.


Ingawa hivyo babu zenu hawakunisikiliza wala kunitegea sikio, lakini walifanya vichwa vyao kuwa vigumu, wakakataa kusikia na kufuata maagizo yangu.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Mimi nitaleta juu ya muji huu na juu ya vijiji vyote vinavyokuwa kandokando yake hasara zote nilizotangaza juu yake, kwa sababu wakaaji wake ni wenye mioyo migumu, nao wamekataa kusikia maneno yangu.


Niliwaazibu ninyi lakini ilikuwa bure, ninyi munakataa maonyo. Muliwateketeza manabii wenu kwa upanga kama simba mwenye uchu.


Ndiyo maana manyunyu yamezuizwa kuanguka, wala mvua za mwisho hazijanyesha. Hata hivyo unakausha macho kama kahaba, wala hauna haya hata kidogo.


Wewe unapanga kwa hekima na unafanya maajabu; njia za watu wote ziko wazi mbele yako, unamulipa kila mumoja kadiri ya njia zake na matendo yake.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwenda uwaambie watu wa inchi ya Yuda na wakaaji wa Yerusalema hivi: Ninyi hamuwezi kupokea mafundisho na kusikia maneno yangu? –Ni ujumbe wa Yawe!


Mpaka hivi leo hamujajinyenyekeza wala kuogopa wala kuzifuata sheria zangu na masharti yangu nilizowawekea ninyi na babu zenu.


Lakini hawakunisikiliza wala kunitegea sikio, lakini wakazidi kufanya vichwa vyao kuwa vigumu na kuasi kuliko hata babu zenu.


Basi utawaambia: Ninyi ni taifa ambalo halikutii sauti ya Yawe, Mungu wao, wala kukubali maonyo yake. Kwenu uaminifu umekufa; umetoweka kabisa katika vinywa vyenu.


Mbona basi, watu hawa wameacha njia inayokuwa sawa na kuendelea katika upotovu wao? Wanashikamana na miungu yao ya uongo, na kukataa kunirudilia mimi!


Watu hao ni wenye kichwa nguvu na moyo mugumu. Ninakutuma kwao, nawe utawaambia: “Bwana wetu Yawe anasema hivi.”


Ewe Yerusalema, matendo yako machafu yamekuchafua. Ingawa nilijaribu kukutakasa, mwenyewe ulibaki muchafu. Basi, hautatakasika tena mpaka nitakapotuliza hasira yangu juu yako.


Umetuazibu kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, lakini mpaka sasa, ee Yawe, Mungu wetu, hatukuomba musamaha wako kwa kuziacha zambi zetu na kutambua uaminifu wako.


Kama hata kisha azabu hiyo bado hamunigeukii mimi, lakini munazidi kupingana nami,


Niliwaletea ugonjwa mukali kama ule nilioupelekea Misri. Niliwaua vijana wenu katika vita, nikatwaa farasi wenu wa vita. Maiti zilijaa katika kambi zenu, harufu yake mbaya ikajaa katika pua zenu. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Niliwaangusha wamoja kati yenu kwa maangamizi kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora. Wale waliobaki kati yenu, walikuwa kama kijiti kilichookolewa katika moto. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna, nikasababisha ukosefu wa chakula popote. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Watu wa miji miwili au mitatu wakakimbilia katika muji mwingine, wapate maji, lakini hayakuwatoshelea. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Niliwapiga pigo la ukosefu wa maji na ukungu; nikakausha bustani na mashamba yenu ya mizabibu; nzige wakakula miti ya tini na mizeituni yenu. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nilisema: Hakika katika muji huu watanitii na kukubali kuonywa; hawataacha kukumbuka mara hizo zote nilizowaazibu. Lakini watu wake walizidisha tamaa zao za kufanya matendo yao kuwa upotovu.


Tunajua kwamba Mungu anahukumu kwa haki watu wanaofanya mambo ya namna hiyo.


Na ikiwa wababa zetu wa kimwili walituadibisha, nasi tuliwaheshimu, jambo hilo halionyeshi zaidi kwamba tunapaswa kumuheshimu Baba yetu wa kiroho na kupata kuishi?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ