Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 5:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Mukimbie huko na huko katika Yerusalema, mupeleleze na kujionea wenyewe, muchunguze katika masoko yake. Mukiona hata mutu mumoja anayefuata sheria, mutu anayetafuta ukweli, basi Yawe atausamehe Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 5:1
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye akasema: “Ninaona uchungu na wivu, ee Yawe, Mungu wa majeshi, kwa sababu watu wa Israeli wamevunja agano lako, wakazibomoa mazabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga; ni mimi tu niliyebaki, nami vilevile wananiwinda waniue!”


Yawe anachunga kwa uangalifu ulimwengu wote, kwa kuwapa nguvu wale wanaokuwa waaminifu kwake. Umetenda jambo la kipumbafu, kwa hiyo tangu sasa, utakuwa na vita kila mara.”


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa vyombo vyenye nyuzi nane. Zaburi ya Daudi.


Yawe anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni aone kama kuna yeyote mwenye akili, kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu.


Lakini wote wamekosa, wote wamepotoka pamoja; hakuna anayetenda mazuri, hakuna hata mumoja.


Nani aliyenisaidia kumupinga mutu mwovu? Nani aliyekuwa upande wangu juu ya wabaya?


Watu wengi wanajivunia kuwa wema, lakini mwaminifu wa kweli anapatikana wapi?


Nunua ukweli, wala usiuuzishe; nunua hekima, mafundisho na akili.


Karibu na milango ya kuingilia katika muji, pahali wanapoingilia watu inaita kwa sauti:


Nikaamuka, nikazunguka katika muji, katika barabara na nafasi za makutano, nikimutafuta yule wangu wa moyo. Nilimutafuta, lakini sikumupata.


Hakuna anayemushitaki mwenzake kwa haki, wala anayejitetea kwa ukweli. Munategemea mambo ya bure; munasema uongo. Munafanya mipango ya kuleta hasara na kuzaa uovu.


Kwa nini basi munanilalamikia? Ninyi wote mumeniasi. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kisha, wanaume wote waliojua kwamba wake wao walikuwa wameifukizia miungu mingine ubani, na wanawake wote waliokuwa hapo, kusanyiko kubwa la watu pamoja na Waisraeli waliokuwa wanakaa Patro katika inchi ya Misri walimujibu Yeremia:


Mimi nilisikiliza kwa uangalifu, lakini wao hawakusema ukweli wowote. Hakuna mutu anayetubu uovu wake, wala kujiuliza hivi: Nimefanya nini? Kila mumoja wao anashika njia yake, kama farasi anavyokimbia haraka kwa vita.


Ndimi zao ni hatari kama pinde; wameimarika kwa ajili ya uongo na si kwa ajili ya haki. Wanaendelea kutenda uovu kisha uovu, wala hawanitambui mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Ndimi zao ni kama mishale yenye sumu, hawachoki kudanganya; kila mutu anaongea vema na jirani yake, lakini anafanya mipango ya kumushambulia ndani ya moyo wake.


Nilitafuta kati yao mutu mumoja atengeneze ukuta na kusimama juu ya nafasi iliyobomoka mbele yangu, kusudi ailinde inchi na kunizuia nisiiharibu, lakini sikumupata hata mumoja.


Naye akaniambia: Uovu wa Waisraeli na watu wa Yuda ni mukubwa sana. Inchi imejaa umwagaji wa damu na katika muji hakuna haki, kwa maana wanasema: Yawe ameiachilia inchi; Yawe haoni.


Lakini sasa, Danieli, weka kwa siri mambo hayo; funga kitabu na kutia muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho utakapofika. Wengi watakimbilia huko na huko, na maarifa yataongezeka.


Wanashambulia muji, wanakimbia juu ya ukuta; wanapanda juu ya nyumba na kuingia, wanapenya katika madirisha kama wezi.


Watu watatangatanga kutoka bahari hata bahari, kutoka upande wa kaskazini mpaka wa mashariki. Watakimbia huko na huko wakitafuta neno la Yawe, lakini hawatalipata.


Nami nikauliza: Watu hawa wanakuja kufanya nini? Yeye akanijibu: Watu hawa wamekuja kuyatisha na kuyaangamiza yale mataifa yenye nguvu ambayo yaliishambulia inchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.


Basi yule mutumishi akarudia na kumwelezea bwana wake maneno hayo yote. Halafu bwana wa nyumba akakasirika, na kumwambia: ‘Kwenda upesi katika nafasi za mukutano na katika barabara za muji, uwalete wamasikini, vilema, vipofu na viwete na kuwaingiza humu.’


Atatumia ubaya wa kila namna kwa kuwadanganya wale wanaopotea kwa sababu hawakupenda kukubali na kupenda mambo ya kweli yaliyoweza kuwaokoa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ